Papa Gregori I

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Papa Gregori I.
Gregori akishughulikia muziki mtakatifu.
Mchoro wa Andrea Mantegna juu ya Gregori akiwa na Yohane Mbatizaji, Benedikto wa Nursia na Jeromu.
Papa Gregori I.
Kaburi la Gregori I, ndani ya Basilica la Mt. Petro huko Vaticano.

Papa Gregori I (takriban 54012 Machi 604) alikuwa papa kuanzia 3 Septemba 590 hadi kifo chake. Alimfuata Papa Pelagio II.

Jina lake la kuzaliwa pia lilikuwa Gregorius. Kutokana na umuhimu wake katika historia, hasa ya Kanisa na Italia, aliongezewa lile la Magnus, yaani "Mkuu".

Lakini mwenyewe, aliposikia kuwa Patriarki wa Konstantinopoli alijiita "Patriarki wa ekumene", aliitikia kwa kujiita "Servus servorum Dei" (yaani "Mtumishi wa watumishi wa Mungu"), jina linalotumiwa hata leo na kila Papa.

Yaliyomo

[hariri] Maisha

[hariri] Utoto na ujana

Gregori alizaliwa mwaka 540 hivi katika familia maarufu ya Anici, akiwa mtoto wa seneta Gordianus na wa Silvia.

Alipokuwa na umri wa miaka 25 tu alichakuliwa kuwa mkuu wa jiji la Roma.

[hariri] Mmonaki na balozi wa papa

Akivutiwa na mfano wa Benedikto wa Nursia, aligeuza nyuma yake mjini kuwa monasteri na kujifanya mmonaki, halafu akajitahidi katika maisha ya sala na kutafakari Biblia.

Lakini mapema papa Pelagio II alimtuma kwenye ikulu la Konstantinopoli, alipobaki miaka sita kama balozi.

[hariri] Upapa

Aliporudi Roma, mwaka 586, akarudia umonaki, lakini tarehe 3 Septemba 590 alishangiliwa na umati wa watu awe papa wa 64.

Mapema alijitokeza kama mtendaji bora hata upande wa jamii na siasa (kwa sababu hiyo aliitwa "Mrumi wa mwisho"), ingawa alikuwa na afya mbovu.

Aliwasiliana viongozi wa nchi mbalimbali za Ulaya, ha Wafranki akafanikisha uongofu wa Uingereza, alipomtuma Augustino wa Canterbury, priori wa monasteri yake ya Sant'Andrea.

Alilinda pia Roma dhidi ya uvamizi wa Agilulf, mfalme wa Walombardi, ambao alijenga nao uhusiano mpya ili kuwaleta kwenye Kanisa Katoliki kutoka uzushi wa Ario, kama alivyofanya na walioendelea kufuata dini za jadi.

Alipambana na matatizo mengine ya Italia, kama vile mafuriko, njaa, tauni, akisimamia kwa usawa masuala ya kijamii yaliyopuuziwa na wawakilishi wa kaisari.

Alishughulikia huduma ya maji.

Alirekebisha liturujia ya Kiroma, akipanga matini ya zamani na kutunga mapya, pamoja na kushughulikia muziki wa ibada ambao kwa heshima yake unaitwa wa Kigregori.

Barua zake 848 zilizotufikia pamoja na hotuba zinashuhudia kazi zake nyingi na ujuzi wake wa Biblia.

Alifariki tarehe 12 Machi 604.

Inawezekana kusema ndiye papa wa kwanza kutumia mamlaka upande wa siasa pia, lakini bila ya kuweka pembeni majukumu yake ya kiroho.

[hariri] Maandishi yake

[hariri] Vyanzo

  • Cantor, Norman F. (1993). The Civilization of the Middle Ages. New York: Harper. 
  • Cavadini, John, ed. (1995). Gregory the Great: A Symposium. Notre Dame: University of Notre Dame Press. 
  • Dudden, Frederick H. (1905). Gregory the Great. London: Longmans, Green, and Co. 
  • Ekonomou, Andrew J. 2007. Byzantine Rome and the Greek Popes: Eastern influences on Rome and the papacy from Gregory the Great to Zacharias, A.D. 590-752. Lexington Books.
  • Richards, Jeffrey (1980). Consul of God. London: Routelege & Keatland Paul. 
  • Straw, Carole E. (1988). Gregory the Great: Perfection in Imperfection. Berkeley: University of California Press. 
  • Leyser, Conrad (2000). Authority and Asceticism from Augustine to Gregory the Great. Oxford: Clarendon Press. 
  • Markus, R.A. (1997). Gregory the Great and His World. Cambridge: University Press. 
  • Ricci, Cristina (2002). Mysterium dispensationis. Tracce di una teologia della storia in Gregorio Magno. Rome: Centro Studi S. Anselmo. . Studia Anselmiana, volume 135.

[hariri] Viungo vya nje

Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine