Papa Gregori I
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Gregori I (takriban 540 – 12 Machi 604) alikuwa papa kuanzia 3 Septemba 590 hadi kifo chake. Alimfuata Papa Pelagio II.
Jina lake la kuzaliwa pia lilikuwa Gregorius. Kutokana na umuhimu wake katika historia, hasa ya Kanisa na Italia, aliongezewa lile la Magnus, yaani "Mkuu".
Lakini mwenyewe, aliposikia kuwa Patriarka wa Konstantinopoli alijiita "Patriarka ya ekumene", aliitikia kwa kujiita "Servus servorum Dei" (yaani "Mtumishi wa watumishi wa Mungu"), jina linalotumiwa hata leo na kila Papa.
Yaliyomo |
[hariri] Maisha
[hariri] Utoto na ujana
Gregori alizaliwa mwaka 540 hivi katika familia maarufu ya Anici, akiwa mtoto wa seneta Gordianus na wa Silvia.
Alipokuwa na umri wa miaka 25 tu alichakuliwa kuwa mkuu wa jiji la Roma.
[hariri] Mmonaki na balozi wa papa
Akivutiwa na mfano wa Benedikto wa Nursia, aligeuza nyuma yake mjini kuwa monasteri na kujifanya mmonaki, halafu akajitahidi katika maisha ya sala na kutafakari Biblia.
Lakini mapema papa Pelagio II alimtuma kwenye ikulu la Konstantinopoli, alipobaki miaka sita kama balozi.
[hariri] Upapa
Aliporudi Roma, mwaka 586, akarudia umonaki, lakini tarehe 3 Septemba 590 alishangiliwa na umati wa watu awe papa wa 64.
Mapema alijitokeza kama mtendaji bora hata upande wa jamii na siasa (kwa sababu hiyo aliitwa "Mrumi wa mwisho"), ingawa alikuwa na afya mbovu.
Aliwasiliana viongozi wa nchi mbalimbali za Ulaya, ha Wafranki akafanikisha uongofu wa Uingereza, alipomtuma Augustino wa Canterbury, priori wa monasteri yake ya Sant'Andrea.
Alilinda pia Roma dhidi ya uvamizi wa Agilulf, mfalme wa Walombardi, ambao alijenga nao uhusiano mpya ili kuwaleta kwenye Kanisa Katoliki kutoka uzushi wa Ario, kama alivyofanya na walioendelea kufuata dini za jadi.
Alipambana na matatizo mengine ya Italia, kama vile mafuriko, njaa, tauni, akisimamia kwa usawa masuala ya kijamii yaliyopuuziwa na wawakilishi wa kaisari.
Alishughulikia huduma ya maji.
Alirekebisha liturujia ya Kiroma, akipanga matini ya zamani na kutunga mapya, pamoja na kushughulikia muziki wa ibada ambao kwa heshima yake unaitwa wa Kigregori.
Barua zake 848 zilizotufikia pamoja na hotuba zinashuhudia kazi zake nyingi na ujuzi wake wa Biblia.
Alifariki tarehe 12 Machi 604.
Inawezekana kusema ndiye papa wa kwanza kutumia mamlaka upande wa siasa pia, lakini bila ya kuweka pembeni majukumu yake ya kiroho.
[hariri] Maandishi yake
- Hotuba 40 kuhusu Injili ni zake kwa hakika, pamoja na 22 juu ya Ezekieli na 2 juu ya Wimbo Ulio Bora)
- Majadiliano - juu ya maisha ya Benedikto wa Nursia
- Maadili kuhusu Ayubu - ufafanuzi wa Kitabu cha Yobu
- Kanuni ya Kichungaji - mpango wa maisha na kazi kwa maaskofu
- Barua 848
[hariri] Viungo vya nje
- Maandishi yote katika mkusanyo "Patrologia Latina" ya Migne
- Papa Gregori I katika Kamusi Elezo ya Kikatoliki
|
|
|---|
| Atanasi • Efrem • Ilari • Sirili wa Yerusalemu • Basili • Gregori wa Nazianzo • Ambrosi • Jeromu • Yohane Krisostomo • Augustino • Sirili wa Aleksandria • Leo • Petro Krisologo • Gregori Mkuu • Isidori • Yohane wa Damasko • Beda • Petro Damiani •
Anselmi • Bernardo • Alberto • Antoni wa Padua • Bonaventura • Thoma wa Akwino • Katerina • Teresa wa Yesu • Petro Kanisio • Yohane wa Msalaba • Roberto Bellarmino • Laurenti wa Brindisi • Fransisko wa Sales • Alfonso Maria • Teresa wa Mtoto Yesu |
| Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Papa Gregori I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |