Papa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kwa samaki anayeitwa kwa Kiswahili kwa neno "papa" tazama papa (samaki)
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
StPetersBasilicaEarlyMorning.jpg
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria
Kukingiwa dhambi ya asili Kupalizwa
Dhambi Purgatorio


Muundo

Papa: Benedikto XVI
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa liturujia
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Milano Lyon Toledo)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Kigiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Papa ni cheo cha kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki duniani kote. Cheo hiki kinaenda sambamba na askofu wa Roma. Kuna orodha ya mapapa.

Yaliyomo

[hariri] Asili ya cheo cha Papa

Kiasili neno la Kiitalia "Papa" lamaanisha "Baba", nalo likawa cheo kwa nia ya kumtaja askofu wa Roma kwa heshima ya pekee. Msingi wa heshima hii ni imani ya kuwa askofu wa Roma ni mwandamizi wa Petro mtume wa Yesu. Wakatoliki huamini ya kwamba Petro alipewa na Yesu kazi ya kuongoza kanisa kwa niaba yake na ya kwamba jukumu hilo linaendelea kati ya waandamizi wa Petro kwenye kiti cha askofu wa Roma.

[hariri] Majina ya mapapa

Papa huchaguliwa na makardinali wa kanisa katoliki baada ya mtangulizi wake kufa au kujiuzulu. Baada ya kuchaguliwa papa mpya anaweza akapata jina jipya. Tangu 2005 ni Papa Benedikto XVI, ambaye awali aliitwa Joseph Ratzinger.

Majina ya mapapa wengine wa kanisa katoliki yapatikana katika orodha ya mapapa.

[hariri] Mkuu wa Vatikano

Papa ni pia mkuu wa nchi ya Mji wa Vatikano iliyopo ndani ya mji wa Roma (Italia).

[hariri] Cheo cha "Papa" penginepo

Cheo cha Papa hutumiwa pia na baadhi ya madhehebu mengine ya Kikristo kwa viongozi wao hasa kwa mkuu wa Kanisa la Kikopti huko Misri.


StPetersDomePD.jpg Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.