Liturujia ya Milano
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Liturujia ya Milano ni liturujia maalumu ambayo inafuatwa katika sehemu kubwa ya jimbo la Milano (Italia) na katika parokia kadhaa za majimbo ya kandokando, hadi lile la Lugano (Uswisi).
Kama asili yake anatajwa babu wa Kanisa Ambrosi, aliyekuwa askofu wa jimbo hilo katika sehemu ya mwisho wa karne ya 4. Ndiyo sababu inaitwa Liturujia ya Ambrosi.
Ingawa Wakatoliki wa maeneo hayo wanafuata liturujia hiyo, upande wa sheria za Kanisa hawatofautiani na wenzao wa Kanisa la Kilatini.