Mlolongo wa Kitume
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mlolongo wa Kitume unasadikiwa kupitia tendo la maaskofu kumwekea mtu mikono kichwani na kumuombea katika kumpatia daraja takatifu.
Mlolongo wa Kitume (kwa Kiebrania האפיפיור הירושה, kwa Kigiriki Αποστολική διαδοχή) ni imani ya baadhi ya madhehebu ya Ukristo, ya kwamba ni lazima viongozi wa Kanisa washiriki mamlaka ya Mitume wa Yesu katika mlolongo usiokatika wa kuwekewa mikono na maaskofu katika kumpatia daraja takatifu.
Imani hiyo inatiwa maanani hasa na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, lakini pia Waanglikana na wengineo.
Kwao, maaskofu wa leo ni waandamizi wa wale wa jana na juzi hata kurudia kwa wale waliowekewa mikono na mitume wenyewe katika karne ya kwanza.
Mlolongo huo unahakikisha uhalali wa mamlaka yao katika kufundisha, kutakasa na kuongoza.
Vyanzo na viungo vya nje [hariri]
- Against Heresies, Online-text, Irenaeus, Against Heresies
- Apostolicity in the Catholic Encyclopedia
- Christian Cyclopedia article on apostolic succession
- Methodist Apostolicity by Gregory S. Neal
- Methodist Episcopacy: In Search of Holy Orders (1990) by Gregory S. Neal
- Scott Hahn on the Papacy by Scott Hahn. Discusses "the chamberlain of the royal household of ancient Israel" or "Prime minister" of the "house of David" (Isaiah 22:22) vis-à-vis Dynastic Succession .
- Views on apostolic succession at WikiChristian
- "Was Wesley Ordained By Bishop Erasmus?" The Methodist Quarterly Review (1878)