Kardinali
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kardinali ni cheo cha juu katika Kanisa Katoliki.
Yaliyomo |
[hariri] Wenye kumchagua Papa
Mkutano wa makardinali humchagua Papa mpya ambaye ni mkuu wa kanisa hili ambayo ni madhehebu ya Kikristo kubwa kuliko jumla ya mengine yote duniani. Uchaguzi hutokea baada ya papa aliyetangulia kufa au kujiuzulu. Kati ya kifo cha papa na uchaguzi wa mwandamizi wake ni mkutano wa makardinali unaoongoza kanisa lote kwa muda. Lakini kardinali aliyefikia umri wa miaka 80 hashiriki tena katika uchaguzi wa Papa.
[hariri] Uteuzi wa kardinali
Kwa kawaida kardinali huteuliwa kati ya maaskofu lakini kuna pia makasisi wachache wanaoteuliwa na papa kuwa kardinali bila ya kupewa uaskofu.
Mwenye kuteua kardinali ni papa peke yake, naye ana haki ya kumteua kardinali bila ya kutangaza jina lake. Kardinali ya aina hii huitwa kwa Kilatini "in pectore" (moyoni). Hii inaweza kutokea hasa kama ni kardinali kutoka nchi pasipo na uhuru wa kidini au nchi ambayo haina uhusiano mzuri na kanisa katoliki.
[hariri] Wajibu wa kardinali
Wajibu kubwa ni wakati wa kifo cha Papa kumchagua mwandamizi wake.
Kuna idadi ya makardinali wanaoishi Vatikani. Kwa kawaida viongozi wa idara za Vatikani wapewa kofia ya kardinali.
[hariri] Idadi ya makardinali
Hakuna idadi maalumu ya makardinali na mnamo 24 Novemba 2007 wako 201. Lakini Papa Paulo VI aliunda utaratibu kuwa wasiwepo zaidi ya makardinali 120 wenye haki ya kupiga kura. Wale waliofikia umri wa miaka 80 hawashiriki tena katika uchaguzi wa papa mpya. Lakini kardinali hajiuzulu wala kustaafu: anaendelea na cheo na pia na haki ya kushiriki katika mkutano wa makardinali hadi kifo.
Kimapokeo makardinali wengi ni Waitalia, hata mapapa walikuwa Waitalia watupu kwa karne nne hadi Papa Yohane Paulo II. Lakini asilimia ya makardinali Waitalia imepungua; kabla ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia zaidi ya nusu walikuwa Waitalia, siku hizi ni takriban asilimia 20. Kwa sasa makardinali wanatokea nchi 70 za mabara yote. Kati yao wenye haki ya kupiga kura wanatokea nchi 52.
Mgawanyo wa makardinali kwenye mabara ni kama ufuatao:
- Afrika - 18
- Amerika ya Kaskazini - 20
- Amerika ya Kusini - 34
- Asia - 21
- Pasifiki - 4
- Ulaya - 104
[hariri] Tazama pia