Asia
Kutoka Wikipedia
Asia ni bara kubwa kabisa kuliko mabara yote mengine ya dunia. Bara hili lina eneo la kilomita za mraba 44,579,000 (maili za mraba 17,212,000), ambalo ni sawa na asilimia 30% ya ardhi yote. Wakazi wa bara la Asia ni 3,701,000,000 kwa mujibu wa makisio 2003.
Bara la Asia lina nchi 44 na visiwa mbali mbali vya madola mbalimbali. Mlima mrefu kabisa ulimwenguni ambao ni mlima wa Everesti wenye urefu wa mita 8,850 (futi 29,035) ulioko Nepal pia uko kwenye bara hili. Kadhalika, nchi zenye wakazi wengi zaidi ulimwenguni China na India pia ziko kwenye bara hili.
Ziwa kubwa kabisa ulimwenguni, bahari ya Kazwini (Caspian Sea) lenye eneo la kilomita za mraba 394,299 (maili za mraba 152,239) vile vile liko Asia kati ya ya nchi hizi: Azerbaijan, Urusi, Kazakhstan, Turkmenistan, na Uajemi.
Bara la Asia linaweza kugawanywa katika sehemu zifuatazo:
Yaliyomo |
[hariri] Asia ya Kati
Sehemu hiyo ya Asia ina nchi saba:
[hariri] Asia ya Kaskazini
Sehemu hiyo ya Asia ina sehemu ya nchi moja tu:
[hariri] Asia ya Mashariki
Sehemu hiyo ya Asia ina nchi nne:
- Uchina (pamoja na Taiwan)
- Japani
- Korea Kaskazini
- Korea Kusini
[hariri] Asia ya Kusini-Mashariki
Sehemu hiyo ya Asia ina nchi kuminamoja
- Brunei
- Indonesia
- Kamboja
- Laos
- Malaysia
- Myanmar (zamani iliitwa Burma)
- Philippines
- Singapur
- Thailand (zamani iliitwa Siam)
- Timor Mashariki
- Vietnam
[hariri] Asia ya Kusini
Sehemu hiyo ya Asia ina nchi saba:
[hariri] Asia ya Magharibi
- Armenia
- Azerbaijan
- Bahrain
- Georgia
- Irak
- Israel
- Kuwait
- Libanon
- Omani
- Palestina
- Qatar
- Syria (pia: Shamu)
- Uarabuni wa Saudia
- Uajemi (au Iran au Persia)
- Uturuki
- Yemeni
- Yordani

