Yordani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
المملكة الأردنية الهاشمية
Al-Mamlakah al-Urduniya al-Hāšimiya

Ufalme wa Kihashemi wa Yordani
Bendera ya Yordani Nembo ya Yordani
Bendera Nembo
Wito la taifa: {{{national_motto}}}
Wimbo wa taifa: عاش المليك
' ash al-malik   
"Heri kwa mfalme"
Lokeshen ya Yordani
Mji mkuu Amman
31°57′ N 35°56′ E
Mji mkubwa nchini Amman
Lugha rasmi Kiarabu
Serikali Ufalme wa Kikatiba
Abdullah II
Samir Rifai
Uhuru
Tarehe

25 Mei 1946
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
92,342 km² (ya 112)
--
Idadi ya watu
 - Julai 2005 kadirio
 - 2003 sensa
 - Msongamano wa watu
 
5,350,000 (ya 106)
4,755,000
64/km² (ya 131)
Fedha Dinar ya Yordani (JOD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
UTC+2 (UTC+2)
UTC+3 (UTC+3)
Intaneti TLD .jo
Kodi ya simu +962



Yordani (pia: Jordan, Jordani Kiar.; الأردنّ }} "al-urdun") ni ufalme wa Kiarabu katika Mashariki ya Kati. Jina rasmi ni Ufalme wa Kihashemi wa Yordani (Kiar.: المملكة الأردنية الهاشمية ) kutokana na familia ya kifalme. Imepakana na Syria, Iraq, Saudi Arabia na Israel. Ina pwani fupi kwenye Ghuba ya Aqaba ya Bahari ya Shamu.

Mji Mkuu ni Amman. Jina la nchi limetokana na mto Yordani ambao ni mpaka wake upande wa magharibi na Israel na eneo la Palestina ya leo.

Sehemu kubwa ya nchi ni jangwa.

Historia [hariri]

Nchi ilianzishwa kwa jina la "Transjordan" (ng'ambo ya mto Yordani) kama sehemu ya eneo la Palestina lililotawaliwa na Uingereza kwa niaba ya Shirikisho la Mataifa baada ya 1918. Waingereza waliamua kutanganisha eneo na Palestina upande wa magharibi ya mto Yordani na kuiweka tangu 1921 chini ya mamlaka ya Abdullah bin al-Husayn wa familia ya Wahashemi aliyekuwa mtoto wa Sharif wa Makka wa mwisho kabla ya kutwaliwa kwa mji huu na Wasaudi. Kwa hatua hii Uingereza ililenga kuimarisha uhusiano wake na makabila ya Waarabu wa jangwa. Abdullahi alitawala awali kwa cheo cha emir baadaye kama mfalme wa "Transjordan".

Jeshi lake lilishiriki katika vita ya mgawanyo wa Palestina na Israel 1948/1949 na kushika sehemu ya Palestina isiyotawaliwa na Israel. Baada ya vita ya siku sita ya 1967 maeneo yote upande wa magharibi ya mto Yordani yalipotelewa na mfalme Hussein mfuasi wa Abdallah tangu 1952 mwishowe aliacha madai yote ya utawala juu ya sehemu hizi.

Viungo vya nje [hariri]

Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Japan | Kambodia | Kazakhstan | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Kirgizstan | Laos | Lebanon | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Urusi1 | Saudia | Singapore | Sri Lanka | Syria | Taiwan (Jamhuri ya China) | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Ufilipino | Uthai | Uturuki1 | Turkmenistan | Uhindi | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi hii iko Asia lakini kwa sababu za kihistoria au kiutamaduni inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya. 3. Eneo la pekee la China.


BlankAsia.png Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Yordani kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.