Pakistan

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jhamhuri ya Kiislamu ya Pakistani
اسلامی جمہوریۂ پاکستان
Islāmī Jamhūriya-i-Pākistān
Bendera ya Pakistani Nembo ya Pakistani
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Iman, Ittehad, Tanzim
(Kiurdu: "Imani, Umoja, Nidhamu")
Wimbo wa taifa: Pak sarzamin shad bad
Lokeshen ya Pakistani
Mji mkuu Islamabad
33°40′ N 73°10′ E
Mji mkubwa nchini Karachi
Lugha rasmi Kiurdu, Kiingereza
Serikali Jamhuri ya Kiislamu
Shirikisho la Jamhuri
Arif Alvi
Shehbaz Sharif
Uhuru
Abbasiya
Dola la Ghazni
Ufalme wa Ghor
Usultani wa Delhi
Dola la Moghul
imetangazwa
Jamhuri
kutoka Uingereza
711-962
9621187
1187-1206
1210-1526
1526-1707
14 Agosti 1947
23 Machi 1956
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
881,912 km² (ya 36)
3.1
Idadi ya watu
 - 2015 kadirio
 - Msongamano wa watu
 
199,085,847 (ya 6)
260.08/km² (ya 55)
Fedha Rupia (Rs.) (PKR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
PST (UTC+5:00)
haipo (UTC+6:00)
Intaneti TLD .pk
Kodi ya simu +92

-


Ramani ya Pakistan
Ramani ya Pakistan

Pakistani ni nchi ya Asia ya Kusini. Imepakana na Ghuba ya Uarabuni upande wa kusini, Afuganistani na Uajemi upande wa magharibi, Uhindi upande wa mashariki na Uchina kaskazini-mashariki.

Mipaka yake na Uhindi na Uchina haitambuliki kimataifa. Pakistan na Uhindi zote mbili zinadai eneo la Kashmir zikitawala kila moja sehemu za eneo hili.

Jina la Pākistān lina maana ya "nchi ya watu safi" kwa Kiurdu.

Pakistani ina nafasi ya sita kati ya nchi duniani zenye watu wengi.

Ni nchi yenye Waislamu wengi duniani baada ya Indonesia.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Wakati wa ukoloni[hariri | hariri chanzo]

Pakistani ilikuwa sehemu ya Uhindi wa Kiingereza hadi 1947.

Mwaka 1857 Wahindi walipinga utawala wa Kampuni ya Kiingereza kwa Uhindi wa Mashariki. Matokeo yake utawala ulishikwa na serikali yenyewe ya Uingereza kama koloni (1858).

Mwisho wa karne ya 19 harakati za Wahindi kutafuta uhuru zilianza upya. Mwaka 1885 chama cha INC (Indian National Congress) kiliundwa na Wahindu na Waislamu pamoja waliodai uhuru.

Mwaka 1906 viongozi Waislamu walitoka katika INC na kuunda "Shirikisho la Waislamu".

Mwaka 1917 Uingereza ulitamka ya kwamba ulitaka kuelekea polepole hali ya kujitawala kwa Wahindi. Viongozi wa wenyeji hawakuridhika na mkasi wa mabadiliko. Chini ya uongozi wa Mahatma Ghandi mwendo wa kupigania uhuru bila mabavu ulipata nguvu. Ghandi alipigania hasa umoja wa Wahindu na Waislamu lakini alipingwa na viongozi wenye itikadi kali wa pande zote mbili.

Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia Waingereza walikubali kujiondoa katika Uhindi. Swali kubwa lilikuwa kama nchi itabaki kama nchi moja au kama maeneo ya Waislamu yatajitenga.

Baada ya uhuru[hariri | hariri chanzo]

Tarehe 14/15 Agosti 1947 utawala wa Uingereza ulikwisha. Bara Hindi iligawanywa katika nchi mbili za Uhindi na Pakistan. Mgawanyo wa Uhindi ulikuja na vita na kumwaga kwa damu nyingi.

Tarehe 30 Januari 1948 Ghandi mwenyewe aliuawa na Hindu mkali aliyemchukia kwa sababu alitaka usawa wa Waislamu na Wahindu.

Wakati ule ilikuwa nchi moja pamoja na Bangla Desh ya leo, lakini mwaka 1971 hizo pande mbili zilitengana baada ya vita kati yao.

Utawala[hariri | hariri chanzo]

Nchi ni shirikisho la majimbo manne ya Punjab, Sindh, Jimbo la mpaka wa kaskazini-magharibi na Baluchistan, mbali ya maeneo matatu.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Lugha rasmi nchini Pakistan ni Kiurdu na Kiingereza. Lugha nyingine ni zaidi ya 60, lakini ni ndogo, zenye wasemaji wachache; karibu zote ni lugha za Kihindi-Kiulaya (angalia orodha ya lugha za Pakistan). Robo tatu za wakazi wanaelewa Kiurdu.

Asilimia 96.4 za wakazi ni Waislamu, hasa Wasuni. Ndiyo dini rasmi. Wahindu ni 2.14% na Wakristo 1.27%.

National symbols of Pakistan (Official)
National animal
National bird
National tree
National flower
National heritage animal
National heritage bird
National aquatic marine mammal
National reptile
National amphibian
National fruit
National mosque
National mausoleum
National river
National mountain

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Pakistan kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.