Kampuni ya Kiingereza kwa Uhindi ya Mashariki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bendera ya Kampuni ya Kiingereza kwa Uhindi wa Mashariki tangu 1801

Kampuni ya Kiingereza kwa Uhindi wa Mashariki ilianza mwaka 1600 kama shirika ya binafsi ya biashara kati ya Uingereza na Uhindi ikaendelea kuchukua utawala juu ya sehemu kubwa ya nchi hadi kuwa serikali kuu ya maeneo karibu yote ya Bara Hindi (Uhindi, Pakistan na Bangla Desh ya leo) mpaka mwaka 1857.

Utawala wa kampuni uliporokoa katika uasi wa askari Wahindi wa jeshi lake mwaka 1857. Mwaka 1858 mali na madaraka ya kiutawala ya kampuni yalichukuliwa na serikali ya Ufalme wa Maungano iliyoendelea kutawala Uhindi kama koloni lake.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kampuni ya Kiingereza kwa Uhindi ya Mashariki kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.