Urusi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kwa matumizi mengine ya jina hili tazama Urusi (Zanzibar)
Российская Федерация
Rossiyskaya Federatsiya

Shirikisho la Urusi
Flag of Russia Nembo ya Russia
Bendera Nembo
Wito la taifa: none
Wimbo wa taifa: Hymn of the Russian Federation
Lokeshen ya Russia
Mji mkuu Moscow
55°45′ N 37°37′ E
Mji mkubwa nchini Moscow
Lugha rasmi Kirusi
Serikali Jamhuri, Shirikisho
serikali ya kiraisi
Dmitry Medvedev
Vladimir Putin
Uhuru
{{{established_events}}}
{{{established_dates}}}
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
17,075,400 km² (ya 1)
13
Idadi ya watu
 - 2006 kadirio
 - 2002 sensa
 - Msongamano wa watu
 
142,400,000 (ya 7)
145,164,000
8.3/km² (ya 209)
Fedha Rubl (RUB)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+2 to +12)
(UTC+3 to +13)
Intaneti TLD .ru, (.su reserved)
Kodi ya simu +7
Alama ya kimataifa ya magari +{{{vehicle_code}}}
1 Rank based on April 2006 IMF data

Urusi (Россия Rossiya) ni nchi ya Ulaya ya Mashariki na Asia. Mji mkuu ni Moscow. Ni nchi kubwa duniani kieneo. Kuna wakazi 144,000,000. Eneo lake ni 17,075,400 km².

Hadi 1991 Urusi ilikuwa sehemu ya Umoja wa Kisovyeti na kiini chake. Wakati ule iliitwa Shirikisho la Jamhuri ya Kisovyiet ya Kijamii ya Kirusi.

Urusi ilikuwa udikteta chini ya chama cha kikomunisti. Tangu 1990 imekuwa demokrasia. Muundo wa serikali ni shirikisho la jamhuri chini ya rais mtendaji.

Yaliyomo

[hariri] Jiografia

Urusi imepakana na Norway, Ufini, Estonia, Latvia, Lithuania, Poland, Belarus, Ukraine, Georgia, Azerbaijan, Kazakhstan, China, Mongolia na Korea ya Kaskazini. Iko karibu vilevile na maeneo ya Marekani (jimbo la Alaska iko ngambo ya mlango wa Bering na Japani (kisiwa cha Hokkaido kiko ng'ambo ya mlango wa La Pérouse.

Eneo la Shirikisho la Kirusi linajumlisha sehemu kubwa ya kaskazini ya mabara ya Ulaya na Asia. Umbali kati ya upande wa magharibi na upande mashariki kabisa ni karibu kilomita 8,000. Mkoa wa Kaliningrad haufuatani moja kwa moja na maeneo mengine ya Urusi umetengwa nayo na nchi za Kibaltiki.

Mara nyingi Urusi hutazamiwa kama sehemu mbili za Urusi wa Ulaya hadi milima ya Ural na Siberia au Urusi wa Kiasia ambayo ni nchi pana kati ya Ural na Pasifiki.

Sehemu kubwa ya Urusi ni tambarare penye vilima vidogo tu. Milima mirefu kuna katika kusini na mashariki ya Siberia.

[hariri] Mito

Kati ya mito mikubwa kuna

[hariri] Miji mikubwa ya Urusi

Majiji mawili makuu ni Moscow na Sankt Peterburg. Sankt Peterburg ilikuwa mji mkuu kuanzia mwaka 1703 hadi 1918 kama makao makuu ya tsar au kaisari wa Urusi. 1924-1989 ikaitwa Leningrad kwa heshima ya kiongozi wa mapinduzi. Moscow ni mji mkuu wa kale iliyorudishwa nafasi yake baada ya mapinduzi ya kikomunisti ya 1918.

Miji mingine mikubwa ni pamoja na

[hariri] Hali ya hewa

Sehemu kubwa za Urusi huwa na vipindi vya majira tofauti sana; joto kubwa inafuatana na baridi kali.

Kaskazini ya Siberia ina ardhi iliyoganda milele maana yake baridi imeingia katika ardhi kabisa. Wakati wa joto sentimita za juu zinapoa na mimea kama manyasi na maua inastawi lakini hakuna miti mikubwa kwa sababu nusu mita chini ya ardhi halijoto inakaa daima chini ya =.

[hariri] Historia

Historia ya Urusi kama nchi ya pekee ilianza polepole pale ambako makabila ya wasemaji wa Kislavoni cha Mashariki walipoanza kujenga maeneo yao kuanzia karne ya 8 BK. Waskandinavia waliunda dola la kwanza katika eneo la Kiev wakaitawala kama dola la Kislavoni. Wenyewe waliingia haraka katika lugha na utamaduni wa wenyeji lakini waliacha jina lao kwa sababu "Rus" kiasili ilikuwa jina kwa ajili ya Waskandinavia wale kutoka Uswidi ya leo. Mwaka 988 Kiev ilipokea Ukristo wa Kiorthodoksi kutoka Bizanti. Dola la Kiev iliporomoka kutokana na mashambulio ya Wamongolia baada ya Jingis Khan na maeneo madogo zaidi yalijitokeza yaliyopaswa kukubali uwana wa Wamongolia.

Kubwa kati ya maeneo yale madogo ilikuwa utemi wa Moscow. Watemi wa Moscow walichukua nafasi ya kwanza kuunganisha Wasalvoni wa Mashariki dhidi ya Wamongolia na kupanusha utawala wao. Baada ya anguko la Konstantinopoli 1453 watawala wa Moscow walipokea cheo cha Kaisari wa Roma kilichoitwa "tsar" na kuwa cheo cha watawala wa Urusi hadi 1917.

Hadi karne ya 18 eneo ya Moscow ilikuwa tayari kubwa likabadilika kuwa Milki ya Kirusi iliyoendelea kupanua katika Siberia na Asia ya Kati.

(inaendelea)

[hariri] Tovuti

Europe.svg Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Urusi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Nchi na maeneo ya Ulaya
Albania | Andorra | Austria | Belarus | Bosnia na Herzegovina | Bulgaria | Kroatia | Denmark | Eire | Estonia | Ufaransa | Hungaria | Iceland | Italia | Jamhuri ya Masedonia | Latvia | Liechtenstein | Lithuania | Luxemburg | Malta | Moldova | Monako |Montenegro | Norway | Poland | Romania | San Marino | Serbia3 | Slovakia | Slovenia | Hispania | Ubelgiji | Uceki | Ufalme wa Muungano (Uingereza) | Ufini | Ugiriki | Ujerumani | Uholanzi | Ureno | Urusi1 | Uswidi | Uswisi | Ukraine | Vatikani

Maeneo ya Ulaya ya kujitawala chini ya nchi nyingine: Visiwa vya Faroe | Gibraltar | Guernsey | Jan Mayen | Jersey | Isle of Man | Svalbard

Nchi za Asia ambazo ni mwanachama wa baraza la Ulaya au vyombo vingine vya Ulaya: Armenia2 | Azerbaijan1 | Kupro2 | Georgia1 | Kazakhstan1 | Uturuki1

Nchi zisizokubaliwa na umma wa kimataifa: Abkhazia | Nagorno-Karabakh2 | Ossetia ya Kusini | Transnistria | Jamhuri ya Kituruki ya Kupro ya Kaskazini2

Maelezo: (1) nchi ya kimabara katika Asia na Ulaya; (2) nchi katika eneo la Asia ya Magharibi lakini kiutamaduni huhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya; (3) Inaelekea kugawiwa kuwa nchi mbili za Serbia na Montenegro

Lugha nyingine