Vatikani
Kutoka Wikipedia
|
|||||
| Wito la taifa: | |||||
| Wimbo wa taifa: Inno e Marcia Pontificale (Kiitalia) Wimbo la Papa |
|||||
| Mji mkuu | Mji wa Vatikani1 |
||||
| Mji mkubwa nchini | Mji wa Vatikani | ||||
| Lugha rasmi | Kilatini2, Kiitalia | ||||
| Serikali | Ufalme Papa Benedikto XVI Tarcisio Kardinali Bertone |
||||
| Uhuru Mkataba wa Laterani |
11 Februari 1929 |
||||
| Eneo - Jumla - Maji (%) |
0.44 km² (ya 232) |
||||
| Idadi ya watu - 2005 kadirio - Msongamano wa watu |
783 (ya 229) 1,780/km² (ya 6) |
||||
| Ethnic groups ([[{{{Ethnic_groups_year}}}]]) | {{{Ethnic_groups}}} | ||||
| Fedha | Euro (€)4 (EUR) |
||||
| Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
CET (UTC+1) CEST (UTC+2) |
||||
| Intaneti TLD | .va | ||||
| Kodi ya simu | +395 |
||||
Mji wa Vatikani ni dola-mji na nchi ndogo kabisa duniani yenye eneo la 0,44 km² pekee. Iko ndani ya mji wa Roma. Ni nchi ya Papa ambaye ni mkuu wa Kanisa Katoliki duniani. Jina limetokana na kilima cha Vatikani (Kilatini: Mons Vaticanus) ndani ya eneo la Roma. Hali halisi ni eneo la kanisa la Mt. Petro, jumba la Vatikani pamoja na majengo na bustani ya jirani. Idadi ya wakazi wa kudumu ni takriban 700 hadi 800.
Pamoja na jengo la Kanisa hilo kubwa kuliko yote duniani, Vatikani ina majengo ya ofisi za utawala wa Kanisa Katoliki, nyumba za kuishi na makumbusho yenye hazina kubwa za sanaa kiasi kwamba nchi nzima inahesabiwa na Umoja wa Mataifa kuwa sanaa.
Yaliyomo |
[hariri] Historia
[hariri] Mabaki ya Dola la Papa
Mji wa Vatikani ni mabaki ya Dola la Papa lililotawala sehemu kubwa za Italia ya Kati kwa karne nyingi hadi 1870. Tangu 1860 maeneo haya yalitwaliwa na Ufalme mpya wa Italia iliyojaribu kuunganisha sehemu zote za rasi ya Italia ndani yake. Utawala wa Papa juu ya mji wa Roma ulilindwa na Ufaransa hadi 1870. Vita ya 1870 kati ya Ujerumani na Ufaransa ililazimisha Ufaransa kuondowa wanajeshi wake Roma na jeshi la Italia likatwaa Roma tar. 20 Septemba 1870. Wakati ule serikali ya Italia ilitaka kumpa Papa Pius IX sehemu ya mji wa Roma katika mazingira ya kilima cha Vatikani kama eneo lake lakini Pius alikataa akitumaini Wakatoliki wa Italia na duniani watalazimisha serikali ya Italia kumrudishia mji wote.
[hariri] Mkataba wa Laterani 1929
Kwa miaka 57 mapapa walijifunga ndani ya jumba la Vatikani. Mwaka 1929 serikali ya Mussolini ilitafuta amani na Papa Pius XI aliyekuwa tayari kukubali mabadiliko. Mkataba wa Laterani wa 11 Februari 1929 ikampa Papa mamlaka na madaraka ya nchi huria juu ya kanisa la Mt. Petro pamoja na eneo jirani.
[hariri] Serikali
Mkuu wa Dola ni papa mwenyewe kwa sasa Benedikto XVI (Josef Ratzinger). Nafasi yake ni kama mfalme asiyebanwa na katiba au masharti yoyote. Mambo ya utawala yako mkononi mwa gavana anayeteuliwa na papa pia.
Vatikani ina Polisi na jeshi lake. Jeshi ni kikosi cha Walinzi Waswisi ambacho kipo tangu mwaka 1506 chenye wanajeshi 100. Wote ni Wakatoliki Waswisi. Inasemekana ni jeshi dogo kabisa lakini pia lenye umri mkubwa kabisa duniani.
Kuna hata Posta ya Vatikani.
|
Va 1euro sede.gif
Euro ya Vatikani |
|||

