San Marino
Kutoka Wikipedia
|
|||||
| Wito la taifa: Latin: Libertas ("Uhuru") |
|||||
| Wimbo wa taifa: Inno Nazionale della Repubblica (sauti pekee bila maneno) | |||||
![]() |
|||||
| Mji mkuu | San Marino |
||||
| Mji mkubwa nchini | Serravalle | ||||
| Lugha rasmi | Kiitalia | ||||
| Serikali
Watawala wakuu(Capitani Reggenti)
|
Jamhuri Gianfranco Terenzi na Loris Francini |
||||
| Uhuru imeundwa |
Septemba 3, 301 | ||||
| Eneo - Jumla - Maji (%) |
61 km² (190th) kidogo sana |
||||
| Idadi ya watu - Januari 2006 kadirio - Msongamano wa watu |
30,002 (ya 190) 481/km² (ya 13) |
||||
| Ethnic groups ({{{Ethnic_groups_year}}}) | {{{Ethnic_groups}}} | ||||
| Fedha | Euro (€) (EUR) |
||||
| Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
CET (UTC+1) CEST (UTC+2) |
||||
| Intaneti TLD | .sm | ||||
| Kodi ya simu | +378 (0549 kutoka Italia) |
||||
San Marino ni kati ya nchi ndogo kabisa duniani. Eneo lake limo ndani ya Italia. San Marino inatajwa kuwa jamhuri yenye umri mkubwa duniani. Ilianzishwa na Wakristo waliokimbia mateso chini ya Kaisari Mroma Diokletiano wakitafuta mkimbilio mlimani.
San Marino ina miji 9. Eneo lake liko kati ya mikoa ya Italia ya Rimini na Pesaro na Urbino karibu na mwambao wa Adria. Eneo lote la 61 km² ni la milima.
[hariri] Siasa
San Marino imetunza utaratibu wa serikali inayofanana na muundo wa jamhuri ya Roma ya kale. Serikali inaongozwa na watawala wawili (Capitani Reggenti) wanaochaguliwa kwa muda wa miezi sita kama zamani konsuli wa Kiroma.
Bunge inaitwa Halmashauri Kuu (Consiglio Grande e Generale) ikichaguliwa kila baada ya miaka mitano. Halmashauri inateua pia kamati ya 12 (Consiglio dei XII) inayotekeleza kazi ya mahakama.
Wananchi wote hukutana mara mbili kwa mwaka kama mkutano mkubwa wa "Arengo" wakiamua juu ya matamko na mapendekezo kwa serikali.


