Hungaria

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Hungaria
Magyarország
Bendera ya Hungaria Nembo ya Hungaria
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: --
Wimbo wa taifa: Himnusz ("Isten, áldd meg a magyart")
"Wimbo" ("Mungu wabariki Wahungaria wote")
Lokeshen ya Hungaria
Mji mkuu Budapest
47°26′ N 19°15′ E
Mji mkubwa nchini Budapest
Lugha rasmi Kihungaria (Magyar)
Serikali Serikali ya kibunge Jamhuri
Tamás Sulyok
Viktor Orbán
Uhuru
Principality of Hungary
Ufalme wa Hungaria
Kuachana kwa
Milki ya Austria-Hungaria
Jamhuri ya Hungaria

896
Desemba 1000

1918
1989
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
93,030 km² (ya 109)
0.74%
Idadi ya watu
 - 2024 kadirio
 - 2023 sensa
 - Msongamano wa watu
 
9,580,000 (ya 95)
9,599,744
103/km² (ya 78)
Fedha Forint ya Hungaria (HUF)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
CEST (UTC+2)
Intaneti TLD .hu 1
Kodi ya simu +36
1 pia .eu kama nchi ya Umoja wa Ulaya


Hungaria (kwa Kihungaria Magyarország) ni nchi ya Ulaya ya Kati yenye wakazi milioni 10 wanaozidi kupungua.

Imepakana na Austria, Slovakia, Ukraine, Romania, Serbia, Kroatia na Slovenia.

Mji mkuu ni Budapest. Miji mingine muhimu ni Miskolc, Debrecen, Szeged, Pécs, Győr na Szolnok.

Kihungaria ndiyo lugha rasmi na ya kawaida kwa wananchi.

Wakazi walio wengi (52.9%) ni Wakristo. hasa Wakatoliki (37.4%) na Wakalvini (11.1%).

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Historia[hariri | hariri chanzo]

Historia ya awali[hariri | hariri chanzo]

Hungaria ilitokea kama nchi ya pekee wakati wa karne ya 10 BK.

Tangu zamani za kuzaliwa kwake Kristo (milenia ya kwanza) sehemu kubwa ya Hungaria ilijulikana kama Panonia ikawa sehemu ya Dola la Roma.

Tangu kuporomoka kwa nguvu ya Waroma ilivamiwa na makabila mbalimbali kama vile Wagermanik, Wahunni na Waslavi.

Baada ya mwaka 900 Wahungaria chini ya mtemi Arpad walivamia eneo hili. Wakati ule Wahungaria walikuwa mkusanyiko wa makabila wahamiaji waliojiita "Majari" (Magyar) waliotoka katika maeneo kati ya mto Volga na milima ya Ural.

Kutoka makazi yao mapya katika Panonia waliendelea kuvamia maeneo mengine ya Ulaya hadi milima ya Pirenei.

Baada ya kupokea Ukristo[hariri | hariri chanzo]

Baada ya kushindwa na Wajerumani mwaka 955 walibaki katika makazi yao na mnamo mwaka 1000 mfalme Ishtvan (Stefano wa Hungaria) alipokea ubatizo akaongoza taifa lake kuingia katika Ukristo.

Wakati wa uvamizi wa Wamongolia baada ya Chingis Khan katika karne ya 13 nchi iliangamizwa, na nusu ya wakazi wakauawa.

Baadaye wafalme Wahungaria waliwakaribisha walowezi kutoka Ujerumani walioanzisha vijiji vingi na pia miji.

Wakati wa karne ya 15 Waturuki Waosmani walianza kuenea kwenye Balkani, wakaingia katika Hungaria kutoka upande wa mashariki. Katika mapigano ya Mohacs mwaka 1526 Hungaria ilishindwa na sehemu kubwa ikawa chini ya Waosmani. Magharibi ya nchi ikaendelea kuitwa ufalme wa Hungaria lakini ufalme uliingia mikononi mwa nyumba ya Habsburg yaani chini ya watawala wa Austria.

Katika karne zilizofuata watawala wa Habsburg walirudisha Waosmani nyuma na ufalme wa Hungaria ukawa sehemu ya milki ya Habsburg yaani Austria.

Katika karne ya 19 mnamo 1848 Wahungaria waliasi dhidi ya watawala lakini walishindwa. Hata hivyo Kaisari Franz Joseph I alibadilisha siasa yake akatafuta usaidizi wa Wahungaria katika utawala wa ufalme. Katiba mpya iliunda cheo cha sawa kati ya Austria na Hungaria chini ya mtawala yeye yule mwenye vyeo vya Kaisari wa Austria na Mfalme wa Hungaria na milki ikaitwa "Austria-Hungaria".

Austria-Hungaria ilikuwa milki kubwa katika Ulaya ya Kati na Mashariki kuanzia mwaka 1867 hadi 1918.

Kuanzia karne ya 20[hariri | hariri chanzo]

Baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia milki ikaporomoka na Hungaria ikaendelea kama nchi ya pekee yenye katiba ya ufalme lakini bila mfalme.

Katika vita kuu ya pili ya dunia Hungaria ikaingia upande wa Ujerumani ukaendelea kuwatesa Wayahudi wake wa kushikamana na siasa ya Hitler na mwishowe ikashindwa pamoja na Ujerumani. Hungaria ikavamiwa na jeshi la Umoja wa Kisovyeti na mabwana hao wapya walihakikisha ya kwamba chama cha kikomunisti ilishika serikali. Hivyo Hungaria ikawa sehemu ya Mapatano ya Warshawa ikasimama upande wa mashariki katika kipindi cha vita baridi.

Mwaka 1956 wananchi wengi walipindua serikali ya kikomunisti na serikali mpya chini ya Imre Nagy ilianzisha demokrasia ya vyama vingi. Lakini wanajeshi wa Kisovyeti wakaingia kati wakarudisha utawala wa chama cha kikomunisti ulioendelea hadi kuporomoka kwa ukomunisti mnamo 1989.

Hungaria imekuwa nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu 2004.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hungaria kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.