Karne ya 13
Lango la Historia | Lango la Biografia | Karibuni | Orodha ya Miaka
◄ | Karne ya 11 | Karne ya 12 | Karne ya 13 | Karne ya 14 | Karne ya 15 | ►
Miaka ya 1200 | Miaka ya 1210 | Miaka ya 1220 | Miaka ya 1230 | Miaka ya 1240 | Miaka ya 1250 | Miaka ya 1260 | Miaka ya 1270 | Miaka ya 1280 | Miaka ya 1290
Karne ya 13 ilikuwa kipindi cha miaka mia moja kati ya 1201 na 1300. Kikamilifu kilianza tarehe 1 Januari 1201 na kuishia 31 Desemba 1300. Namba zake zinafuata hesabu ya miaka "baada ya Kristo".
Kama kila "karne" ni kipindi kinachohesabiwa kwa hiari ya kibinadamu kwa sababu ni mgawanyo wa kalenda tu: katika hali halisi maendeleo na mabadiliko makubwa hayafuati migawanyo ya kalenda ya kibinadamu.
Kuna mambo mengi yaliyotokea wakati wa karne hii, kama haya yafuatayo.
Watu na matukio [hariri]
| Karne: Karne ya 12 | Karne ya 13 | Karne ya 14 |
| Miongo na miaka |
| Miaka ya 1200 | 1200 1201 1202 1203 1204 1205 1206 1207 1208 1209 |
| Miaka ya 1210 | 1210 1211 1212 1213 1214 1215 1216 1217 1218 1219 |
| Miaka ya 1220 | 1220 1221 1222 1223 1224 1225 1226 1227 1228 1229 |
| Miaka ya 1230 | 1230 1231 1232 1233 1234 1235 1236 1237 1238 1239 |
| Miaka ya 1240 | 1240 1241 1242 1243 1244 1245 1246 1247 1248 1249 |
| Miaka ya 1250 | 1250 1251 1252 1253 1254 1255 1256 1257 1258 1259 |
| Miaka ya 1260 | 1260 1261 1262 1263 1264 1265 1266 1267 1268 1269 |
| Miaka ya 1270 | 1270 1271 1272 1273 1274 1275 1276 1277 1278 1279 |
| Miaka ya 1280 | 1280 1281 1282 1283 1284 1285 1286 1287 1288 1289 |
| Miaka ya 1290 | 1290 1291 1292 1293 1294 1295 1296 1297 1298 1299 |
- Gengis Khan (1162 - 1227), anaanzisha kipindi cha pax mongolica, Ulaya inafanya biashara na China
- Konstantinopoli unatekwa na watu wa Ulaya magharibi: mwanzo wa Ufalme wa Kilatini wa mashariki
- Miji yenye bahari ya Italia inatawala Bahari ya Mediteranea, hasa Venezia
- Zinaanza benki
- Falme za kitaifa zinajitokeza Ulaya
- Kaisari Federik II anastawisha sanaa akitawala huko Palermo (Sisilia)
- Papa Inosenti III anafikisha mamlaka ya Papa upande wa siasa kwenye kilele chake
- Inastawi sanaa ya Kigoti
- Ukoo wa Wapaleologi unakomboa Konstantinopoli na kuleta hali mpya ya ustawi
- Marko Polo (Venezia, 1254 - 1324), mfanyabiashara na mvumbuzi huko China
- Fransisko wa Asizi (Asizi, 1182 hivi - 1226), mwanzilishi wa Wafransisko
- Dominiko wa Guzman kuanzisha shirika la Wahubiri
- Toma wa Akwino (1225 hivi - 1274), anafikisha elimu ya Skolastika kwenye kilele chake
- Huko Cina wanabuni dira