Moldova

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Moldova


Moldova ni nchi ya Ulaya ya Mashariki.

Inapakana na Ukraina na Romania.

Eneo lake ni la km2 33,843, ingawa Transnistria imejitenga kwa msaada wa Urusi.

Mji mkuu ni Chișinău.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Kwa kiasi kikubwa historia ya Moldova inahusiana na ile ya Romania kwa kuwa ni taifa moja kwa utamaduni, lugha na dini.

Baada ya vita vikuu vya kwanza Moldova ilikuwa sehemu ya Umoja wa Kisovyeti kwa jina la Jamhuri ya Kisovyeti ya Kijamii ya Kimoldova hadi ilipopata uhuru wake tarehe 27 Agosti 1991.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Wakazi ni milioni 3.5 hivi.

Lugha rasmi ni Kiromania, ambacho kimetokana hasa na Kilatini. Ni lugha ya kwanza ya 76% ya wakazi wote, ikifuatwa na Kirusi (16%).

Upande wa dini, 93.34% ni Wakristo Waorthodoksi.

Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Moldova kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.