Ucheki
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
|
|||||
| Wito la taifa: Pravda vítězí (Kicheki: "Ukweli hushinda") |
|||||
| Wimbo wa taifa: Kde domov můj | |||||
![]() |
|||||
| Mji mkuu | Praha |
||||
| Mji mkubwa nchini | Praha | ||||
| Lugha rasmi | Kicheki | ||||
| Serikali | Jamhuri Václav Klaus Mirek Topolánek |
||||
| ' Kutokea kwa taifa Uhuru kutoka Austria-Hungaria Mwisho wa Chekoslovakia |
Karne ya 9 (Dola la Moravia) 28 Oktoba 1918 1 Januari, 1993 |
||||
| Eneo - Jumla - Maji (%) |
78,866 km² (ya 117) 2.0 |
||||
| Idadi ya watu - 2006 kadirio - 2001 sensa - Msongamano wa watu |
10,265,231 (ya 78) 10,230,060 130/km² (ya 77) |
||||
| Fedha | Koruna (CZK) |
||||
| Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
CET (UTC+1) CEST (UTC+2) |
||||
| Intaneti TLD | .cz 3 | ||||
| Kodi ya simu | +4201 |
||||
Ucheki (Kicheki: Česko) pia Jamhuri ya Kicheki au Jamhuri ya Czechia (Kicheki: Česká republika) ni nchi ya Ulaya ya Kati na mwanachama wa Umoja wa Ulaya. Imepakana na Poland, Ujerumani, Austria na Slovakia. Mji mkuu ni Praha (Kijer.: Prag; Kiing.: Prague).
Miji mingine mikubwa ni Brno, Ostrava, Zlín, Plzeň, Pardubice, Hradec Králové, České Budějovice, Liberec, Olomouc na Ústí nad Labem.
Tangu zamani nchi imekuwa na kanda mbili za Bohemia, Moravia na Silesia.
Wakazi husema hasa Kicheki ambacho ni lugha ya Kislavoni ya Magharibi.
[hariri] Historia
Kwa sehemu kubwa ya historia yake hadi 1918 Ucheki ilikuwa chini ya watawala wa Habsburg waliokuwa wafalme na makaisari wa Austria. Baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia Ucheki ilipata uhuru pamoja na Slovakia katika nchi ya Chekoslovakia. Mwaka 1993 Ucheki na Slovakia ziliachana na kuwa nchi ya pekee kila moja.
[hariri] Viungo vya Nje
| Makala hiyo kuhusu "Ucheki" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Ucheki kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |


