Kicheki
Kicheki ni lugha ya Kislavoni katika familia ya lugha za Kislavoni cha Magharibi inayotumiwa nchini Ucheki. Kuna wasemaji takriban milioni mbili nje ya Ucheki.
Kicheki ni lugha ya karibu na Kislovakia na Kisorbi. Kinaandikwa kwa alfabeti ya Kilatini.
Wageni hushtuka mara nyingi wakiona maneno bila vokali kwa mfano sentensi "Strč prst skrz krk". Sababu yake ni ya kwamba herufi za r na l zinaweza kuhesabiwa kama silabi (utaratibu unaofanana na "m" kama mwanzo wa neno mbele ya konsonanti katika lugha za Kibantu: m-fano, M-swahili) .
Sarufi inapanga nomino zote katika jinsia tatu.
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.