Kiromania
Kiromania (Kiromania: român tamka "romin") ni kati ya lugha za Kirumi na lugha rasmi ya Romania na Moldova.
Asili ya Kilatini [hariri]
Asili yake ni Kilatini ya Roma ya Kale kwa sababu sehemu kubwa ya Romania ya leo ilikuwa jimbo la Dakia katika Dola la Roma. Leo hii takriban theluthi mbili za msamiati una asili ya Kilatini, asilimia 20 ni za asili ya Kislavoni na mengine kutuoka lugha mbalimbali za jirani kama Kigiriki au Kituruki.
Wasemaji [hariri]
Katika Romania penye wakazi milioni 22 zaidi ya milioni 19 hutumia Kiromania kama lugha ya mama. Nchini Moldova penye wakazi 4.5 karibu milioni 4 husema Kiromania inayoitwa huko "Kimoldova" lakini ni lugha ileile. Kuna pia waesamji katika nchi jirani hasa Serbia, Ukraine, Urusi (Siberia), Bulgaria na Hungaria. Waromania waliohamia huendelea kutumia lugha huko Marekani, Kanada, Australia, Israel au Uturuki. Baada ya mwisho wa ukomnisti waromania wengi wametafuta kazi na kukaa Hispania na Italia.
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.