Mapatano ya Warshawa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

-Mapatano ya Warshawa ni tofauti na mkataba wa Warshawa kuhusu usafiri wa kimataifa kwa ndege-

Mapatano ya Warshawa (Kiing. Warsaw pact) ilikuwa jina la maungano ya kijeshi ya Umoja wa Kisovyeti na nchi 7 za Ulaya wakati wa vita baridi baada ya 1945. Jina rasmi ilikuwa "Mapatano juu ya urafiki, ushirikiano na kupeana usaidizi" na ilitiwa sahihi 1955 mjini Warshawa.

Ilikuwa jibu la Umoja wa Kisovyeti dhidi ya kuundwa kwa NATO upande wa Marekani na nchi za Ulaya ya Magharibi. Ilikwisha pamoja na mwisho wa vita baridi ikaondolewa rasmi 1991.

Wanachama[hariri | hariri chanzo]

Wanachama wa mapatano ya Warshawa 1956 - 1968.

Nchi zote za kikomunisti za Ulaya zilijiunga isipokuwa Yugoslavia.