Uchaguzi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sarafu ya Kiroma ikionyesha upigaji kura

Uchaguzi ni mchakato wa kumteua mtu kwa nafasi maalumu katika jamii, hasa cheo na majukumu yanayotokana nacho.

Uchaguzi hufanyika kwa nafasi za uongozi au nafasi za mamlaka fulani. Uchaguzi hutokea mara nyingi kwa njia ya kupiga kura kwa wenye haki ya kura.

Katika chama, jumuiya binafsi au klabu ni wanachama wanaopigia kura kamati ya uongozi, mwenyekiti na maafisa wengine.

Katika shirika za hisa ni wenye hisa wanaopigia kura uongozi.

Katika dola ni raia au wawakilishi wao wanaochagua. Hapa kuna mbinu tofauti kufuatana na katiba ya nchi.

  • uchaguzi wa viongozi wakuu na raia, pamoja na kiongozi wa taifa (rais), wa serikali (waziri mkuu), wa manisipaa au mkoa, jaji, wabunge
  • uchaguzi wa wawakilishi (kwa mfano wabunge) watakaochagua wenye vyeo wengine
  • mchanganyiko kati ya mbinu mbili za kwanza