Jeromu
Jeromu au Yeronimo (Strido, leo nchini Korasya 347 - Bethlehemu, Israeli, 420) alikuwa padri, mmonaki na mtaalamu wa Biblia, aliyemudu vizuri lugha zote za kitabu hicho pamoja na Kilatini hata akawa mwandishi bora wa lugha hiyo kati ya mababu wa Kanisa.
Tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu na babu wa Kanisa.
Mwaka 1298 Papa Bonifasi VIII alimuongezea sifa ya mwalimu wa Kanisa.
Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 30 Septemba.
Yaliyomo |
Maisha [hariri]
Alizaliwa mwaka 347 huko Strido, sehemu za Dalmazia .
Alisomea Roma miaka ya 360 - 367, akijipatia elimu ya hali ya juu, aliyoiendeleza maisha yake yote, hata kwa safari nyingi magharibi na mashariki zilizomwezesha kufahamiana na watu wengi maarufu.
Alibatizwa huko Roma akiwa na umri wa miaka 25, akaendelea moja kwa moja kupambana kiume na tabia yake ngumu iliyochanganya ukali na wepesi wa kulia machozi, unyofu na elekeo la kinyongo, maisha magumu na hisia kali, uadilifu na hamaki, hisani na uchungu wa maneno.
Akishika kazi, saumu, sala na makesha, alivuta wengi kumfuata Kristo kwa karibu zaidi.
Miaka 375 - 377 katika jangwa la Kalchis alifundishwa Kiebrania na Myahudi aliyeongokea Ukristo.
Mwaka 379 kisha kupewa upadri na askofu Paulino wa Antiokia alikwenda Konstantinopoli alipokamilisha ujuzi wake wa lugha ya Kigiriki chini ya Gregori wa Nazianzo.
Baada ya kuishi kama mmonaki miaka 3 akarudi Roma (382) na kuanza kutafsiri vitabu vya Origene, mpaka alipoteuliwa na Papa Damaso I kuwa karani na mshauri wake.
Wakati huo alikamilisha ujuzi wake wa Kiebrania kwa msaada wa mwalimu wa dini ya Kiyahudi, na baada yake akazidi kutegemea elimu ya Kibiblia ya dini hiyo badala ya mbinu za Origene. Ndiyo sababu alikataa vitabu vya Deuterokanoni.
Baada ya papa huyo kufa (385), upinzani dhidi yake ulizidi, akahamia Mashariki ya Kati, alipoanzisha na kuongoza monasteri kadhaa za kike na za kiume zenye elimu ya hali ya juu, akaishi katika mojawapo huko Bethlehemu, akitafsiri na kufafanua Biblia hadi dakika yake ya mwisho (420).
'Vulgata' [hariri]
Vulgata, tafsiri ya kwanza ya Biblia ya Kikristo nzima katika Kilatini ndiyo kazi yake muhimu zaidi. Aliianza kwa agizo la papa Damaso I mwaka 382, akaimaliza baada ya miaka 23. Tafsiri hiyo ilitumika kama msingi wa tafsiri nyingine nyingi hadi karne XX. Hata hivyo tangu wakati wake ilikosolewa sana kwa kufuata mno msimamo wa Uyahudi.
Pia alitafsiri vitabu vingine, alitunga hotuba, barua pamoja na vitabu juu ya maisha ya watu maarufu (yeye akiwa mmojawao) na vya kupinga mafundisho ya wengine.
Sala yake [hariri]
Ee Bwana, umetupatia Neno lako kama nuru ambayo iangazie njia yetu; utujalie tulitafakari Neno lako na kufuata mafundisho yake hivi kwamba tuone hiyo nuru inazidi kuangaza hadi adhuhuri, kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
Vyanzo [hariri]
- J.N.D. Kelly, "Jerome: His Life, Writings, and Controversies" (Peabody, MA 1998)
- S. Rebenich, "Jerome" (London and New York, 2002)
Viungo vya nje [hariri]
- "St. Jerome" by Louis Saltet, in The Catholic Encyclopedia (1910)
- Jewish Encyclopedia: Jerome
- St. Jerome - Catholic Online
- The Story of St. Jerome and the Lion
- St Jerome (Hieronymus) of Stridonium Orthodox synaxarion
Maandishi kwa Kilatini [hariri]
- Maandishi yake yote katika Patrologia Latina ya Migne pamoja na faharasa
- Chronological list of Jerome's Works with modern editions and translations cited
- Opera Omnia (Maandishi Yote) from Migne edition (Patrologia Latina, 1844-1855) with analytical indexes, almost complete online edition
Google Books' Facsimiles [hariri]
- Migne volume 23 part 1 (1883 edition)
- Migne volume 23 part 2 (1883 edition)
- Migne volume 24 (1845 edition)
- Migne volume 25 part 1 (1884 edition)
- Migne volume 25 part 2 (1884 edition)
- Migne volume 28 (1890 edition?)
- Migne volume 30 (1865 edition)
Tafsiri za Kiingereza [hariri]
- English translations of Biblical Prefaces, Commentary on Daniel, Chronicle, and Letter 120 (tertullian.org)
- Jerome's Letter to Pope Damasus: Preface to the Gospels
- English translation of Jerome's De Viris Illustribus
- The Perpetual Virginity of Blessed Mary
- Lives of Famous Men (CCEL)
- Apology Against Rufinus (CCEL)
- Letters, The Life of Paulus the First Hermit, The Life of S. Hilarion, The Life of Malchus, the Captive Monk, The Dialogue Against the Luciferians, The Perpetual Virginity of Blessed Mary, Against Jovinianus, Against Vigilantius, To Pammachius against John of Jerusalem, Against the Pelagians, Prefaces (CCEL)
|
|||||