Jeromu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Mt. Jeromu alivyochorwa na Caravaggio.

Jeromu au Yeronimo (347-420) alikuwa padri, mmonaki na mtaalamu wa Biblia, aliyemudu vizuri lugha zote za Biblia pamoja na Kilatini.

Anaheshimiwa kama mtakatifu, babu wa Kanisa na mwalimu wa Kanisa.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 30 Septemba.

Yaliyomo

[hariri] Maisha

Alizaliwa mwaka 347 huko Strido, sehemu za Dalmazia (leo Korasya).

Alisomea Roma, mwaka 379 kisha kupewa upadri na askofu Paulino wa Antiokia alikwenda Konstantinopoli alipokamilisha ujuzi wake wa lugha ya Kigiriki chini ya Gregori wa Nazianzo.

Baada ya kuishi kama mmonaki miaka 3 akarudi Roma (382), alipoteuliwa na Papa Damaso I kuwa karani wake.

Baada ya papa huyo kufa, upinzani dhidi yake ulizidi, akahamia Mashariki ya Kati, alipoanzisha monasteri kadhaa za kike na za kiume akaishi katika mojawapo hadi kufa (420).

[hariri] 'Vulgata'

Vulgata, tafsiri ya kwanza ya Biblia ya Kikristo katika Kilatini ndiyo kazi yake muhimu zaidi. Aliianza kwa agizo la papa Damaso I mwaka 382, akaimaliza baada ya miaka 23. Tafsiri hiyo ilitumika kama msingi wa tafsiri nyingine nyingi hadi karne ya 20.

[hariri] Vyanzo

  • J.N.D. Kelly, "Jerome: His Life, Writings, and Controversies" (Peabody, MA 1998)
  • S. Rebenich, "Jerome" (London and New York, 2002)

[hariri] Viungo vya nje

[hariri] Maandishi kwa Kilatini

[hariri] Google Books' Facsimiles

[hariri] Tafsiri za Kiingereza

Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine