Yohane wa Avila

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Mtakatifu Yohane wa Avila.

Yohane wa Avila (ambaye alizaliwa Almodóvar del Campo 6 Januari 1500, akafariki Montilla tarehe 10 Mei 1569) alikuwa padri mwanajimbo wa Hispania aliyeathiri sana Kanisa Katoliki la nchi hiyo na urekebisho wa Kikatoliki katika karne ya 16.

Kwa namna ya pekee mkoa wa Andalusia na watakatifu Teresa wa Yesu, Yohane wa Mungu na Fransisko Borgia walifaidika na utume wake.

Papa Leo XIII alimtangaza mwenye heri tarehe 12 Novemba 1893, halafu Papa Paulo VI akamtangaza mtakatifu tarehe 31 Mei 1970.

Papa Benedikto XVI ametangaza nia ya kumfanya mwalimu wa Kanisa wa 34.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 10 Mei kila mwaka.


Christian cross.svg Makala hii kuhusu Mkristo huyu bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Yohane wa Avila kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine