Mwalimu wa Kanisa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Walimu wa Kanisa)
Walimu wa Kanisa wa kwanza kutangazwa walivyochorwa na Pier Francesco Sacchi mwaka 1516 hivi. Kwa sasa mchoro unatunzwa huko Paris, Ufaransa. Kuanzia kushoto mbele: Agostino wa Hippo, Papa Gregori I, Jeromu na Ambrosi wa Milano.
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo

Papa: Fransisko
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Mwalimu wa Kanisa ni jina la heshima ambalo kwa nadra Kanisa Katoliki linampa mtakatifu ambaye katika maisha, mafundisho na maandishi yake alionyesha na kueneza mwanga wa pekee katika masuala ya imani, maadili na maisha ya kiroho.

“Tamko la kwamba mtakatifu fulani ni Mwalimu wa Kanisa lote linategemea utambuzi wa karama maalumu ya hekima ambayo alijaliwa na Roho Mtakatifu kwa faida ya Kanisa ikabainishwa na athari njema ya mafundisho yake katika Taifa la Mungu” (Papa Benedikto XVI, Barua ya Kitume ya tarehe 7 Oktoba 2012).

Utaratibu[hariri | hariri chanzo]

Jina hilo linatolewa na Papa au Mtaguso. Mpaka sasa, katika miaka karibu 2000 ya historia ya Kanisa wanaume 32 na wanawake 4 tu wamepewa heshima hiyo.

Wa kwanza kutangazwa (mwaka 1298) ni mababu wa Kanisa wanne muhimu zaidi upande wa Magharibi: Ambrosi wa Milano, Agostino wa Hippo, Jeromu na papa Gregori I.

Mwaka 1568 walitangazwa mababu wa Kanisa wanne muhimu zaidi upande wa Ukristo wa Mashariki: Atanasi wa Aleksandria, Basili Mkuu, Gregori wa Nazienzi na Yohane Krisostomo, pamoja na Thoma wa Akwino, mwalimu bora wa Karne za Kati upande wa Ukristo wa Magharibi.

Halafu mapapa wakaendelea kuongeza wengine. Wa mwisho kutangazwa kwa sasa ni Gregori wa Narek (12 Aprili 2015).

Orodha[hariri | hariri chanzo]

Mwaka wa kutangazwa ukifuatwa na nyota unaonyesha watakatifu wanaoheshimiwa na Waorthodoksi pia, ingawa kwao hakuna cheo cha mwalimu wa Kanisa.

Marejeo kwa Kiswahili[hariri | hariri chanzo]

  • Masomo ya Breviari - ed. Ndanda Mission Press - Ndanda 1978
  • Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1989
  • MAURICE SOSELEJE – Kalendari Yetu Maisha ya Watakatifu – Toleo la Pili – ed. Benedictine Publications Ndanda-Peramiho – Ndanda 1986 - ISBN 9976-63-112-X