Bernardo wa Clairvaux
Bernardo wa Clairvaux (Fontaine-lès-Dijon, Ufaransa, 1090 - Ville-sous-la-Ferté, Ufaransa, 20 Agosti 1153) alikuwa abati wa urekebisho wa Citeaux wa shirika la Benedikto wa Nursia.
Ni mtu muhimu zaidi wa karne ya 12 katika Kanisa Katoliki, ambalo linamheshimu kama mtakatifu (alitangazwa na Papa Alexander III mwaka 1174) na mwalimu wa Kanisa (alitangazwa na Papa Pius VIII mwaka 1830).
Ni msimamizi wa wakulima.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 20 Agosti.
Yaliyomo |
[hariri] Maisha
Bernardo alikuwa mtoto wa tatu kati ya saba waliozaliwa na Teshelino na Aleta, wote wa koo bora za watawala wadogo wa Borgogne (Ufaransa).
Alisoma kwa Wakanoni wa Nôtre Dame de Saint-Vorles, karibu na Châtillon-sur-Seine.
Kisha kurudi katika ngome ya baba yake huko Fontaines, mwaka 1111 alitawa pamoja na ndugu zake 5 na jamaa na marafiki kadhaa katika nyumba ya Châtillon, mpaka mwaka uliofuata akajiunga pamoja na wenzake 30 na monasteri ya Cîteaux, iliyoanzishwa miaka 15 ya nyuma na Roberto wa Molesmes. Kwa wakati huo ilikuwa chini ya Stefano Harding.
Mwaka 1115 alihamia pamoja na wamonaki wenzake 12 katika mkoa wa Champagne, walipozawadiwa shamba kubwa karibu na mto Aube, wakaliita Clairvaux, yaani bonde angavu.
Kwa muda mfupi Abasia ya Clairvaux ikawa kivutio kikubwa kwa miito ya utawa hata ikaweza kuanzia mwaka 1118 kutuma wamonaki kuanzisha sehemu nyingine kama vile huko Trois-Fontaines, Fontenay, Foigny, Autun, Laon; Bernardo alipokufa abasia za urekebisho wa Citeaux zilikuwa 343, ambazo 66 kati yake zilianzishwa au kurekebishwa naye.
Maisha yake yote Bernardo akawa mtetezi shujaa wa imani sahihi na wa mamlaka ya Kanisa.
Vita vya msalaba vya mwaka 1147 vilifanikiwa kuungwa mkono na watu wa Ufaransa na pia Ujerumani kutokana na mahubiri yake.
Mwishoni mwa mwaka 1152 alikuwa ameishiwa nguvu, lakini alisafiri hadi Metz ili kutuliza fujo za mji huo.
Aliporudi Clairvaux, akafa tarehe 20 Agosti 1153.
[hariri] Njia ya sala ya Bernardo
Bernardo hakuelekea ujuzi unaotokana na mantiki, bali ule unaopatikana kwa kuzama katika mafumbo katika sala ya kujaliwa. Ndiyo njia pekee ya kumfahamu kweli Mungu na kufikia amani na heri ya kuwa naye.
[hariri] Maandishi
- De consideratione libri quinque ad Eugenium III
- De diligendo Deo
- De gradibus humilitatis et superbiae
- De Gratia et libero arbitrio
- De laude novae militiae ad Milites Templi
- De laudibus Virginis Matris
- Contemplatio Passionis
- Expositio in Canticum Canticorum
- Meditatio super fletus Virginis
- Sermones
- Sermones de tempore
- Sermones super Cantica Canticorum
- Epistola ad Raymundum dominum Castri Ambuosii
- Sermo de miseria humana
- Tractatus de interiori domo seu de conscientia aedificanda
- Varia et brevia documenta pie seu religiose vivendi
- Visio contemplativa
[hariri] Viungo vya nje
- Maandishi yake yote kwa Kilatini kadiri ya Patrologia Latina ya Migne
- San Bernardo e la storia
- Waraka wa Papa Pius XII juu ya Mt. Bernardo
|
|||||