Biblia
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Biblia ni jina la jumla kwa ajili ya vitabu vitakatifu vya dini ya Uyahudi na hasa yaUkristo. Neno limetokana na lugha ya Kigiriki ambayo ndani yake βιβλία biblia ina maana ya "vitabu" ikiwa ni uwingi wa βιβλος biblos. Hii ni kwa sababu Biblia ni mkusanyo wa maandiko mbalimbali yaliyoweza kutungwa kwa muda wa miaka 1000 hivi.
Tunaweza kutofautisha
- Biblia ya Kiebrania au Tanakh inavyotumiwa na Wayahudi. Vitabu hivyo 39 kwa Kanisa Katoliki na wengineo ni sehemu kuu ya vile 46 vinavyoitwa "Agano la Kale" (wakati Wakristo wengine, hasa Waprotestanti, wanakubali hivyo 39 tu). Ndilo sehemu ya kwanza ya
- Biblia ya Kikristo inavyotumiwa na Wakristo yenye vitabu vya Agano la Kale pamoja na Agano Jipya.
[hariri] Viungo vya Nje
Biblia kwa lugha ya Kiswahili (Union Version)