Agano Jipya
Kutoka Wikipedia
Agano Jipya ni sehemu ya pili ya Biblia ya kikristo yenye vitabu 27. Yaleta habari za Yesu Kristo, mitume yake na chanzo cha kanisa la Kikristo.
Yaliyomo |
[hariri] Vitabu vya Agano Jipya
(Kwa mabano: kifupi cha kawaida kwa kutaja kitabu hiki)
[hariri] Vitabu vya kihistoria
Injili nne zasimulia habari za Yesu.
- Injili ya Matthayo (Mt.)
- Injili ya Marko (Mk.)
- Injili ya Luka (Lk.)
- Injili ya Yohane (Yn.)
Historia ya chanzo cha kanisa iko katika
- Matendo ya Mitume (Mdo.)
[hariri] Nyaraka
[hariri] Nyaraka za Paulo
Kuna maandiko 13 kati ya nyaraka yanayomtaja Mtume Paulo kama mwandishi. Wataalamu wa leo hutofautiana kama kweli nyaraka hizi zote zimeandikwa na Paulo mwenyewe. Kwa jumla saba zimetambuliwa na karibu wataalamu wote kuwa ni maandiko yake. Kuhusu mengine kuna maswali kwa sababu mbalimbali (kwa mfano tofauti za lugha, mkazo tofauti ya mafundisho) na wataalamu wengine hudai ya kuwa labda zimeandikwa na wanafunzi wake au na mwandishi kwa niaba ya Paulo.
- Waraka kwa Waroma (Rum.)
- Waraka wa kwanza kwa Wakorinto (1Kor.)
- Waraka wa pili kwa Wakorinto (2.Kor.)
- Waraka kwa Wagalata (Gal.)
- Waraka kwa Waefeso (Efe.)
- Waraka kwa Wafilipi (Flp.)
- Waraka kwa Wakolosai (Kol.)
- Waraka wa kwanza kwa Wathesaloniki (1Thes.)
- Waraka wa pili kwa Wathesaloniki (2Thes.)
- Waraka wa kwanza kwa Timotheo (1Tim.)
- Waraka wa pili kwa Timotheo (2.Tim.)
- Waraka kwa Tito (Tit.)
- Waraka kwa Filemoni (Flm.)
[hariri] Waebrania
- Waraka kwa Waebrania (Ebr.) una tabia ya pekee; tangu zamani ulihesabiwa kuwa waraka wa Paulo lakini ndani yake jina la Paulo halitajwi.
[hariri] Nyaraka katoliki
Jina "katoliki" halimaanisha dhehebu la Kiroma-katoliki lakini maana asilia ya neno la kigriki katoliki ambayo ni "kwa watu wote". Maana yake hazilengi ushirika maalumu au kikundi fulani ndeani ya Ukristo lakini ziliandikwa kwa wakristo wote kwa jumla. Nyaraka hizi zote ziliandikwa katika jina la mtume fulani wa Yesu au Mkristo mwingine wa kanisa la kwanza.
- Waraka wa Yakobo (Yak.)
- Waraka wa kwanza wa Petro (1Pet.)
- Waraka wa pili wa Petro (2Pet.)
- Waraka wa kwanza wa Yohane (1Yoh.)
- Waraka wa pili wa Yohane (2.Yoh.)
- Waraka wa tatu wa Yohane (3Yoh.)
- Waraka wa Yuda (Yud.)
[hariri] Kitabu cha kinabii
- Ufunuo wa Yohane (Ufu.)
[hariri] Viungo vya Nje
Toleo la Agano Jipya kwa Kiswahili

