Kitabu cha Hekima

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kitabu cha Hekima au Hekima ya Solomoni ni cha mwisho kuandikwa (miaka 50 hivi KK) katika ya vitabu vya deuterokanoni vya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.

Hupangwa kati ya vitabu vya hekima, kichwa chake kinavyodokezwa.

Kama vitabu vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Mwandishi[hariri | hariri chanzo]

Ingawa mwandishi anajidai kuwa mfalme Solomoni ili kutia maanani ujumbe wake, wataalamu wanasema lugha fasaha na mawazo vinaonyesha wazi asili yake katika mazingira ya Kigiriki ya Aleksandria (Misri).

Alikuwa Myahudi msomi katika dini, falsafa na maadili.

Uchunguzi makini umeonyesha jinsi mashairi yake yametungwa kwa hesabu kali sana.

Mafundisho[hariri | hariri chanzo]

Kati ya michango yake upande wa teolojia kuna fundisho la kutokufa kwa roho, lakini pia utabiri juu ya mateso ya Yesu na umilele wa Hekima ya Mungu.

Sala ya kujiombea hekima (Hek 9:1-6)[hariri | hariri chanzo]

"Ee Mungu wa baba zetu, Bwana, mwenye kuihifadhi rehema yako,

umevifanya vitu vyote kwa neno lako;

na kwa Hekima yako ukamwumba mwanadamu,

ili avitawale viumbe vilivyoumbwa nawe,

na kumiliki ulimwengu katika utakatifu na kwa haki,

na kutoa hukumu kwa unyofu wa moyo.

Nakusihi unipe Hekima,

ambayo huketi karibu nawe katika kiti chako cha enzi,

wala usinikatae mimi miongoni mwa watumishi wako;

mimi niliye mtumwa wako, na mwana wa mjakazi wako,

mtu dhaifu asiye na siku nyingi,

wala sina nguvu ya kufahamu hukumu na sheria.

Kwa maana mtu ajapokuwa ni mkamilifu miongoni mwa wanadamu,

pasipo Hekima itokayo kwako atahesabiwa kuwa si kitu".

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitabu cha Hekima kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.