Kitabu cha Methali
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kitabu cha Mithali kimo katika Tanakh (Biblia ya Kiebrania, hivyo pia katika Agano la Kale la Biblia ya Kikristo ambamo ni cha kwanza kati ya vitabu vya hekima.
Yaliyomo |
[hariri] Historia yake
Kweli kitabu hicho kinaonekana cha zamani kuliko vile vinavyofuata; labda kilikamilika katika karne ya 4 K.K., kisha kukusanya tafakuri za vizazi kadhaa.
[hariri] Lugha yake
Kitabu kiliandikwa kwa Kiebrania na kutafsiriwa kwa mara ya kwanza katika lugha ya Kigiriki (Septuaginta).
[hariri] Yaliyomo
Yaliyomo ni maadili ambayo yamuongoze mtu maishani ili awe na heri.
[hariri] Ufafanuzi wake
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.
[hariri] Viungo vya nje
Kitabu cha Methali katika tafsiri ya Kiswahili (Union Version)
Mwanzo Kutoka Walawi Hesabu Kumbukumbu Yoshua Waamuzi Ruthu Samueli I Samueli II Wafalme I Wafalme II Mambo ya Nyakati I Mambo ya Nyakati II Ezra Nehemia TobitiDK YudithiDK Esta Wamakabayo IDK Wamakabayo IIDK Yobu Zaburi Methali Mhubiri Hekima DK SiraDK Wimbo Bora Isaya Yeremia Maombolezo BarukuDK Ezekieli Danieli Hosea Yoeli Amosi Obadia Yona Mika Nahumu Habakuki Sefania Hagai Zekaria Malaki - Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.