Kitabu cha Ruthu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ruth katika shamba la Boazi.

Kitabu cha Ruthu ni kimojawapo kati ya vitabu vifupi vya Biblia ya Kiebrania, kwa hiyo pia ya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.

Ni kati ya vile vichache vilivyo na jina la mwanamke ambaye ndiye mhusika mkuu wa habari.

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Umuhimu wake[hariri | hariri chanzo]

Katika fujo ya miaka ya Waamuzi (Kitabu cha Waamuzi), habari ya kitabu hiki kifupi inatujenga: inamhusu Ruthu, mwanamke Mpagani wa kabila la Moabu aliyeolewa na Mwisraeli kwao, ng’ambo ya mto Yordani.

Baada ya kufiwa mume wake akafuatana na mama mkwe Naomi hadi Bethlehemu ili aolewe na ndugu wa marehemu na kumzalia mtoto kadiri ya Torati, sheria ya Israeli.

Baada ya kufanikiwa kuolewa na Boazi kwa msaada wa Naomi, alimzaa Obedi.

Huyo mtoto akawa baba wa Yese na babu wa mfalme Daudi.

Hivyo kwa uaminifu wake mwanamke huyo pia akatajwa katika Injili kama bibi wa Yesu (Math 1:5-6).

Mazingira[hariri | hariri chanzo]

Habari kuu ya kitabu cha Ruthu ilitokea wakati wa Waamuzi, lakini inafurahisha moyo, ikilinganishwa na hali mbaya ya kidini na ya kimaadili iliyoandikwa katika kitabu cha Waamuzi.

Habari yenyewe inaonyesha kwamba imani kamili kwa Mungu na uangalifu na upendo kwa watu wengine wakati ule pia ulikuwepo katika Israeli.

Katika taifa zima walikuwepo watu waliojitahidi kuishi maisha ya unyenyekevu na haki mbele ya Mungu wa kweli.

Habari hiyo pia inaonyesha kwamba Mungu aliwaangalia watu kama hao kwa neema yake kubwa, akiyaongoza mambo yao ya kila siku na kuwafanikisha. Wema huo pia ulikuwa baraka kwa taifa zima.

Yaliyomo[hariri | hariri chanzo]

  • 1:1-22 Miaka kumi ya taabu katika nchi ya Moabu
  • 2:1-4:22 Mwanzo wa maisha mapya katika Israeli

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitabu cha Ruthu kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.