Roberto Bellarmino
Roberto Francesco Romolo Bellarmino alizaliwa Montepulciano (wilaya ya Siena nchini Italia) tarehe 4 Oktoba 1542 akafariki Roma tarehe 17 Septemba 1621.
Alitangazwa na Papa Pius XI kuwa mwenye heri tarehe 13 Mei 1923, mtakatifu tarehe 29 Juni 1930 na mwalimu wa Kanisa tarehe 17 Septemba 1931.
Yaliyomo |
[hariri] Maisha
[hariri] Utoto na ujana
Roberto alizaliwa katika familia kubwa, akiwa mtoto wa kiume wa tatu kati ya watano; wazazi wake walikuwa na asili ya kisharifu, lakini hali ya uchumi ilikuwa tofauti. Baba yake, Vincenzo Bellarmino alikuwa jaji, mama yake, Cinzia Cervini, alikuwa dada wa Papa Marcello II.
Tangu utotoni alikuwa na afya mbovu na mwelekeo mkubwa kwa mambo ya dini kama mama yake. Baada ya kupata malezi nyumbani, alitumwa Padova kwa masomo.
Alipofikia umri wa miaka 18, akifuata wito wake wa upadri, na kuvutiwa na mfano wa Ignas wa Loyola, aliamua kujiunga na Shirika la Yesu alilolianzisha, na tarehe 21 Septemba 1560 aliweka nadhiri zake za kwanza.
Bila ya kujivunia undugu wake na Papa, alidumu kuwa na unyenyekevu na bidii.
Alisomea Roma tangu 1560 hadi 1563, halafu alianza kufundisha Firenze na Mondovì, katika shule za shirika lake.
Mwaka 1567 alianza kusoma kwa mpango teolojia huko Padova, lakini kutokana na sifa yake kama mhubiri, mwaka 1569 mkuu wa shirika, Fransisko Borja, alimtuma Louvain (leo katika Ubelgiji), kwenye chuo kikuu maarufu cha mji huo. Ndipo alifahamu kwa karibu Uprotestanti.
[hariri] Ufundishaji
Baada ya kupata upadrisho huko Gand tarehe 25 Machi 1570, alibaki Louvain miaka sita, hadi 1576 kama mwalimu wa teolojia na mhubiri, akizidi kupata wanafunzi na wasikilizaji kutoka kila upande.
Basi, Papa Gregori XIII alimuita Roma afundishe hoja dhidi ya uzushi, kama alivyofanya hadi mwaka 1587. Ni kwamba Mtaguso wa Trento ulikuwa umemalizika tangu muda mrefu, na Kanisa Katoliki lilikuwa na haja ya kujiimarisha kielimu na kiroho. Kazi ya Roberto iliingia moja kwa moja katika juhudi hizo za Urekebisho wa Kikatoliki.
Kuanzia mwaka 1588, akiwa kiongozi wa kiroho wa Collegio Romano, alishirikiana sana na Papa Sixtus V, ingawa huyo hakumpenda sana yeye wala shirika lake. Kati ya vijana aliowalea, maarufu zaidi ni Alois Gonzaga, ambaye alifariki mwaka 1591 kutokana na tauni aliyoambukizwa na mtu aliyemuokota barabarani. Baada ya kushughulikia kesi ya kumtangaza mwenye heri, aliomba azikwe karibu naye, kama ilivyotokea baadaye. Mwaka 1592 hadi 1594 alikuwa gombera wa seminari hiyo, halafu mwaka 1595 akawa mkuu wa shirika katika kanda ya Napoli.
[hariri] Ukardinali
Mwaka 1597 Papa Klementi VIII alimrudisha Roma kama mshauri katika masuala ya teolojia n.k.
Tarehe 3 Machi 1599 Papa alimteua kuwa kardinali akieleza kwamba, Kanisa la Mungu halina mwingine sawa naye katika elimu. Bellarmino alijaribu kwa kila njia kumfanya Papa abadili msimamo, lakini mwishoni alilazimika kukubali. Pamoja na hayo, hakubadili maisha yake magumu, na mapato yake aliyaelekeza karibu yote kwa maskini.
Kama kardinali aliongoza idara mbalimbali za Papa na kuwa Askofu mkuu wa jimbo la Capua (1602-1605).
Miaka ya mwisho alitunga katekisimu (kubwa na ndogo) iliyoenea sana hadi mwisho wa karne ya 19.
[hariri] Maandishi
Opera omnia zilizokusudia kukusanya maandishi yake yote zilitolewa Cologne (1617), Venezia (1721), Napoli (1856), Paris (1870).
Kati ya yale muhimu zaidi kuna haya yafuatayo: Mabishano:
- Disputationes de Controversiis Christianae Fidei adversus hujus temporis hereticos
- De Exemptione clericorum na De Indulgentiis et Jubilaeo, ambayo yaliingizwa baadaye katika De Controversiis
- De Transitu Romani Imperii a Graecis ad Francos
- Responsio ad praecipua capita Apologiae [...] pro successione Henrici Navarreni
- Judicium de Libro quem Lutherani vocant Concordiae
- Responsio Matthaei Torti ad librum inscriptum Triplici nodo triplex cuneus
- Apologia Bellarmini pro responsi one sub ad librum Jacobi Magnae Britanniae Regis
- Tractatus de potestate Summi Pontificis in rebus temporalibus, adversus Gulielmum Barclay
- Dottrina Cristiana Breve
- Dichiarazione Più Copiosa Della Dottrina Cristiana
- Dichiarazione del simbolo
- Admonitio ad Episcopum Theanensem nepotem suum quae sint necessaria episcopo
- Exhortationes Domesticae
- Conciones habitae Lovanii
- De Ascensione mentis in Deum
- De Aeterna felicitate sanctorum
- De gemitu columbae
- De septem verbis Christi
- De arte bene moriendi
Ufafanuzi wa Biblia na mengineyo:
- De Scriptoribus ecclesiasticis
- De Editione Latinae Vulgatae, quo sensu a Concilio Tridentino definitum sit ut ea pro authenticae habeatur
- In omnes Psalmos dilucida expositio
[hariri] Viungo vya nje
- Matukio ya maisha yake katika Catholic forum web-site.
- Kitabu De Laicis kuhusu serikali katika tafsiri ya Kiingereza
- Kitabu Maneno Saba ya Yesu Msalabani
- Kitabu Heri ya Milele ya Watakatifu
- Kitabu Ufundi wa Kufa Vema)
- Kitabu hichohicho katika PDF
- [1]. Taarifa muhimu juu yake
- [2] Maisha yake.
|
|||||