Sirili wa Yerusalemu
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtakatifu Sirili wa Yerusalemu (315 – 386) alikuwa askofu wa Yerusalemu.
Ametambuliwa kuwa mtakatifu na mwalimu wa Kanisa.
Sikukuu yake ni tarehe 18 Machi.
[hariri] Maisha
Sirili alizaliwa katika familia ya Kikristo mwaka 315.
Aliteuliwa kuwa Askofu wa Yerusalemu nchini Israeli mwaka 348.
Alihusika hasa na mabishano na Ario juu ya umungu wa Yesu, na kwa sababu hiyo zaidi ya mara moja alifukuzwa nchini mwake.
Moyo wake wa kichungaji unaonekana hasa katika kitabu chake Catecheses, ambamo anawaeleza watu mafundisho ya kweli ya Ukristo, Maandiko Matakatifu, na mapokeo ya Kanisa.
Alikufa mwaka 386.
[hariri] Tazama pia
[hariri] Marejeo
- "Sala ya Kanisa - Vipindi vya Liturjia", Toleo la Tatu 1996, Ndanda - Peramiho: Benedictine Publications, uk.1300
|
|
|---|
| Atanasi • Efrem • Ilari • Sirili wa Yerusalemu • Basili • Gregori wa Nazianzo • Ambrosi • Jeromu • Yohane Krisostomo • Augustino • Sirili wa Aleksandria • Leo • Petro Krisologo • Gregori Mkuu • Isidori • Yohane wa Damasko • Beda • Petro Damiani •
Anselmi • Bernardo • Alberto • Antoni wa Padua • Bonaventura • Thoma wa Akwino • Katerina • Teresa wa Yesu • Petro Kanisio • Yohane wa Msalaba • Roberto Bellarmino • Laurenti wa Brindisi • Fransisko wa Sales • Alfonso Maria • Teresa wa Mtoto Yesu |
| Makala hii kuhusu Mkristo huyu bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Sirili wa Yerusalemu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |