Kitabu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Vitabu

Kitabu (Kar. كتاب kitabun) ni mkusanyo wa kurasa zilizofungwa pamoja kwa njia ya kudumu. Siku hizi kitabu kimekuwa hasa mkusanyo wa kurasa za karatasi zilizochapishwa. UNESCO imetoa elezo kuwa kitabu ni tangazo kwa umma lililochapishwa lenye kurasa zisizopungua 49.

Lakini kuna pia vitabu vyenye kurasa tupu vitakavyoandikiwa kwa mkono. Hadi karne ya 15 BK vitabu vyote viliandikwa kwa mkono kwa kutumia kalamu na kwa sababu hii vilikuwa vichache na bei ilikuwa juu. Johannes Gutenberg alibuni mashine ya kuchapisha vitabu iliyofaulu na kurahisisha vitabu sana.

Siku hizi vitabu hutolewa pia kwa njia ya mtandao au CD kama vitabu pepe.

Kitabu kilichochapishwa mara nyingi duniani ni Biblia ya Kikristo imetolewa kwa nakala bilioni 5-6.

Viungo vya Nje [hariri]

Books-aj.svg aj ashton 01.svg Makala hii kuhusu kitabu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitabu kama Mwandishi wake, hadithi au matoleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.