Familia
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kwa matumizi mengine ya neno hili tazama Familia (maana)
Familia ni kundi la watu wanaokaa pamoja kama baba, mama na watoto. Kikundi hiki mara yingi ni sehemu ya kundi kubwa zaidi ya ukoo unaounganisha watu wenye asili katika uzazi wa pamoja.
[hariri] Aina za familia
Aina za familia zinatofautiana duniani kutokana na utamaduni na hali ya jamii.
Katika nchi nyingi za Afrika familia ndogo ya baba, mama na watoto kwa kawaida ni sehemu tu ya familia kubwa zaidi pamoja na ndugu za baba au mama, akina babu na bibi na kadhalika. Lakini hata Afrika kuna taratibu tofauti tofauti kama ni ndugu wa baba au ndugu wa mama wanaotazamiwa kuwa karibu zaidi kwa watoto wa familia ndogo.
Vilevile kuna tofauti kama muundo wa kawaida ni mume mmoja na wake wengi na kila mmoja akiwa na watoto wake tena.
Katika jamii za nchi zilizopita kwenye mapinduzi ya viwandani kama Ulaya na Marekani familia inamaanisha hasa familia ndogo inayokaa pamoja katika nyumba. Ukoo haukupotea lakini umuhimu wake umepungua sana na mara nyingi ni chaguo la watu ndani ya ukoo kama wanapenda kujumiyana na ndugu zao au la.
Katika mazingira ya miji mikubwa au pale ambako koo za kale zimeporomoka na kuachana kuna jumuiya ndogo sana kama mama na watoto ambao ni familia bila baba au wanaume. Aina hii ya familia yenye mzazi mmoja tu imepatikana pia kama familia ya baba na watoto kama utamaduni unamruhusu baba peke yake kulea watoto.
Katika mazingira ya umaskini, vita au mabadiliko ya haraka sana kuna pia watoto wengi wanaoishi kwa bibi au babu na hata hali hii ni aina ya familia.
| Makala hiyo kuhusu "Familia" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Familia kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |