Cape Town

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Jiji la Cape Town

Bendera

Nembo
Jiji la Cape Town is located in Afrika Kusini
Jiji la Cape Town
Jiji la Cape Town
Mahali pa mji wa Cape Town katika Afrika Kusini
Anwani ya kijiografia: 33°55′48″S 18°27′36″E / 33.93°S 18.46°E / -33.93; 18.46
Nchi Afrika Kusini
Majimbo Rasi Magharibi
Tovuti: www.capetown.gov.za
Cape Town inavyoonekana kutoka Mlima wa Meza (nyuma baharini Robben Island alipofungwa Nelson Mandela)
Mlima wa Meza ni ishara ya mji

Cape Town ( "Mji wa rasi"- Kiafrikaans: Kaapstad; Kixhosa: iKapa) ni mji mkubwa wa tatu wa Afrika Kusini na mmoja kati ya miji mikuu mitatu ya nchi ikiwa ni makao ya Bunge. Pia ni mji mkuu wa jimbo la Rasi Magharibi (Western Cape / Wes-Kaap). Ni sehemu ya Jiji la Cape Town. Eneo lake ni 1,644 km² lenye wakazi 2,375,910 (mwaka 2005).

Jina la mji limetokana na Rasi ya Tumaini Jema iliyoko karibu upande wa kusini.

Ni mji wa kwanza katika eneo la Afrika Kusini hivyo huitwa mara nyingi "mji Mama" wa nchi. Kihistoria mji ulianzishwa kama kituo cha mapumziko kwenye njia ya safri kwa meli kati ya Uholanzi na koloni zake huko Asia hasa Indonesia ya leo. Kampuni ya Kiholanzi ya India ya Mashariki ilimtuma Jan van Riebeeck kwenye rasi kusudi aanzishe kijiji ambako vyakula vitalimwa kwa ajili ya mabaharia njiani. Walowezi Waholanzi pamoja na Wajerumani na Wafaransa walifuata. Wakaona wenyeji Khoikhoi wakikataa kuwafanyia kazi walileta watumwa kutoka visiwa vya Indonesia. Hapo ndipo mwanzo wa jumuiya muhimu ya Waislamu wa Cape Town. Tangu mwaka 1814 rasi ilikuwa koloni ya Uingereza.

Cape Town ulikuwa mji mkubwa wa Afrika Kusini hadi kupatikana kwa dhahabu katika eneo la Johannesburg kuanzia 1887.

Cape Town ina uwanja wa ndege wa kimataifa mkubwa wa pili nchini. Ni mji wa Afrika Kusini unaotembelewa na watalii kushinda miji yote mingine. Wengi wanaona iko kati ya miji inayopendeza hasa kote duniani.

Kisiwa cha Robben Island ilikuwa mahali pa gereza alikofungwa Nelson Mandela; leo ni makumbusho yanayotembelewa na maelfu wa watalii kila mwaka.

Ishara ya mji ni Mlima wa Meza unaotazama hori ya Cape Town ukitenganisha kitovu cha mji na makazi ya Cape Flats.

[hariri] Viungo vya Nje

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Government
Habari
Mengine
SouthAfricanStub.png Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Cape Town kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Vifaa binafsi
Maeneo ya wiki

Vibadala
Vitendo
Urambazaji
Vifaa
Lugha zingine