Mashariki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alama za dira zikionyesha mashariki katika hali ya mkoozo (E = "East" = mashariki)

Mashariki ni moja kati ya mielekeo minne mikuu ya dira. Mwelekeo wake ni upande jua linapochomoza asubuhi.

Jina "mashariki" limetokana na neno la Kiarabu مشرق mashriq linalomaanisha "mahali jua linapokucha".

Mashariki kawaida huwa upande wa kulia kwenye ramani. Tanzania ipo mashariki mwa nchi za Kongo, Rwanda na Burundi. Bahari Hindi huwa upande mwa mashariki ya Tanzania na Kenya. Hakuna mwisho wa kuelekea mashariki hadi umezunguka dunia yote.

Kundi la nchi za Asia magharibi mara nyingi huitwa "Mashariki ya Kati" ambayo ni uzoefu kutoka mtazamo wa Ulaya.

Majengo ya makanisa mara nyingi hujengwa kutazama upande wa mashariki kwa kukumbuka kufufuka kwa Yesu kulikotokea wakati wa kucha; kwa hiyo altari ya kanisa huwekwa upande wa mashariki wa kanisa na waumini huangalia upande huu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]


Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.