Bahari ya Hindi
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bahari Hindi)
Bahari ya Hindi ni bahari kubwa ya tatu duniani ikiwa imechukua asilimia 20 ya uso wa dunia. Upande wa kaskazini imepakana na Asia ya Kusini; magharibi imepakana na Ghuba ya Uajemi, Bahari ya Shamu na Afrika; mashariki imepakana na Ghuba ya Malay, visiwa vya Sunda (Indonesia), na Australia; na kusini imepakana na Bahari ya Kusini.
Bahari hii ni njia muhimu ya usafirishaji na usafiri kwa meli kati ya Asia na Afrika.


