Papa Benedikto II

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Benedikto II.

Papa Benedikto II alikuwa Papa kuanzia tarehe 26 Juni 684 hadi kifo chake tarehe 8 Mei 685[1]. Alitokea Roma, Lazio, Italia[2][3].

Jina la baba yake lilikuwa Yohane.

Alimfuata Papa Leo II akafuatwa na Papa Yohane V.

Mwimbaji wa Kanisa tangu utotoni, alijulikana kwa ujuzi wa Biblia na muziki. Pia alipenda ufukara, alikuwa mpole na mnyenyekevu, na kung'aa kwa uvumilivu na huruma kwa wahitaji.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Benedikto II kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.