Papa Agatho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Agatho.

Papa Agatho alikuwa Papa kuanzia tarehe 27 Juni 678 hadi kifo chake tarehe 10 Januari 681[1]. Alitokea Sicilia, Italia[2][3].

Alitetea imani sahihi dhidi ya wazushi waliosema Yesu hakuwa na utashi wa kibinadamu na aliendesha sinodi kadhaa ili kuimarisha umoja wa Kanisa.

Inasemekana kwamba alikuwa na umri wa zaidi ya miaka mia moja alipochaguliwa kuwa Papa, na alikuwa ametunza hazina ya Kanisa kwa miaka mingi[4].

Wakati wa Upapa wake ulifanyika Mtaguso wa tatu wa Konstantinopoli (680-681) uliofundisha rasmi kwamba Yesu, chini ya utashi wake wa Kimungu, alikuwa na utashi wa kibinadamu pia[5].

Alimfuata Papa Donus akafuatwa na Papa Leo II.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Kanisa Katoliki linaadhimisha sikukuu yake tarehe 10 Januari[6], lakini Waorthodoksi tarehe 20 Februari.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  3. Jeffrey Richards (1 May 2014). The Popes and the Papacy in the Early Middle Ages: 476–752. Routledge. p. 270. ISBN 9781317678175. 
  4. Butler, Alban. "St. Agatho, Pope", The Lives of the Saints, Vol. I, 1866.
  5. Hubert Cunliffe-Jones (24 April 2006). A History of Christian Doctrine (reprint ed.). A&C Black. p. 233. ISBN 9780567043931. 
  6. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Agatho kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.