Papa Adeodato I

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Papa Adeodatus I)
Papa Adeodato I.

Papa Adeodato I (pia aliitwa Deusdedit) alikuwa Papa kuanzia tarehe 19 Oktoba 615 hadi kifo chake tarehe 8 Novemba 618[1]. Alitokea Roma, Italia[2]. Jina la baba yake lilikuwa Stephanus, ambaye alikuwa shemasi mdogo.

Alimfuata Papa Bonifasi IV akafuatwa na Papa Bonifasi V.

Kabla ya kuchaguliwa, alitoa huduma ya kipadri kwa miaka 40[3]. Baadaye alikuza idadi ya mapadri na kuwapa nafasi zilizokuwa zimeshikwa na wamonaki kadiri ya sera ya Papa Gregori I na Papa Bonifasi IV[4][3] .

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[6].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  3. 3.0 3.1 Attwater, Aubrey (1939). A Dictionary of Popes: From Peter to Pius XII. p. 66. ISBN 0199295816. 
  4. Jeffrey Richards, The Popes and the Papacy in the Early Middle Ages (London: Routledge and Kegan Paul, 1979), p. 262
  5. Philips, Fr Andrew. The Holy Orthodox Popes of Rome.
  6. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Adeodato I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.