Papa Benedikto VI
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Benedikto VI alikuwa papa kuanzia 19 Januari, 973 hadi kifo chake mwezi wa Julai au Agosti 974. Jina lake la kuzaliwa halijulikani. Alimfuata Papa Yohane XIII. Alilindwa hasa na Mfalme Mkuu Otto I wa Ujerumani. Otto alipofariki, wenyeji wa mji wa Roma walimfunga Benedikto VI na baada ya miezi michache walimuua.

