Papa Gregori XIII

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Gregori XIII.

Papa Gregori XIII (Bologna, Italia, 7 Januari 1502; Roma, 10 Aprili 1585) alikuwa Papa wa Kanisa Katoliki kuanzia tarehe 13/25 Mei 1572 hadi kifo chake[1]. Alitokea Bologna, Italia[2].

Alimfuata Papa Pius V akafuatwa na Papa Sixtus V.

Anakumbukwa hasa kwa matengenezo ya kalenda iliyokuja kujulikana kama "kalenda ya Gregori" ikawa kalenda ya kimataifa kote duniani hadi leo.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa kwa jina la Ugo Buoncampagni akafuata masomo ya sheria na kuwa profesa wa sheria kwenye chuo kikuu cha Bologna.

Mwaka 1539 aliitwa na Papa Paulo III akapewa kazi mbalimbali kama mwanasheria wa Kanisa.

Baadaye Papa Paulo IV alimpa cheo cha askofu wa Viesti (Italia) na ni hapo tu kwamba Ugo alikula kiapo cha upadri na kuwekwa wakfu kama askofu moja kwa moja.

Baada ya kifo cha Papa Pius V alichaguliwa kuwa mwandamizi wake, akachukua jina la "Gregorius".

Papa Gregori XIII alijitahidi kurudisha nyuma mwendo wa matengenezo ya Kiprotestanti. Alikubali dhuluma dhidi ya Wakristo wa Kiinjili nchini Ufaransa tarehe 23 - 24 Agosti 1572 ("Usiku wa Bartolomeo").

Alijaribu kukusanya mataifa ya Ulaya dhidi ya Dola la Uturuki kwa shabaha ya kukomboa mji wa Konstantinopoli lakini hakufaulu.

Pamoja na jitihada hizi za kisiasa alijenga taasisi ya taaluma. Aliunda Chuo Kikuu cha Kipapa huko Roma kinachoitwa kwa heshima yake "Gregoriana" hadi leo.

Kalenda mpya hakuitunga mwenyewe, lakini aliita wataalamu katika kamati maalumu na kukubali mapendekezo waliyotoa tarehe 24 Februari 1582.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Gregori XIII kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.