Papa Fabian

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Fabian na Mtakatifu Sebastian.

Papa Fabian alikuwa Papa kuanzia mwaka 236 hadi kifodini chake tarehe 20 Januari 250[1]. Alitokea Roma, Italia.

Alimfuata Papa Antero akafuatwa na Papa Kornelio.

Alichaguliwa akiwa bado mlei[2], akatoa mfano mtukufu wa imani na maadili.

Aliongoza Kanisa miaka mingi katika hali ya utulivu, hasa chini ya kaisari Filipo Mwarabu ambaye anasemekana alibatizwa naye[3].

Kadiri ya wanahistoria Wakristo[4][5], chini ya kaisari Decius (250 BK), Papa Fabian alituma maaskofu 7 kutoka Roma kwenda Gallia (Ufaransa wa leo) wakahubiri Injili: Grasyano huko Tours, Trofimo huko Arles, Paulo huko Narbonne, Saturnini huko Toulouse, Denis huko Paris, Austremoni huko Clermont na Martial huko Limoges.

Hatimaye alifia dini yake katika dhuluma ya kaisari Decius. Sipriano wa Karthago alisifu ushindi wake na kwamba alitoa kielelezo bora cha uongozi[6].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini[7].

Sikukuu yake ni tarehe 20 Januari[8].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. Attwater, Donald; John, Catherine Rachel (1993). The Penguin Dictionary of Saints (3rd ed.). New York: Penguin Books. ISBN 0-14-051312-4. 
  3.  Chisholm, Hugh, ed. (1911). "Fabian, Saint". Encyclopædia Britannica. 10 (11th ed.). Cambridge University Press. p. 113.
  4. Gregory, Historia Francorum I §30, giving as his source the Martyrdom of Saturnin.
  5. The Vetus Martyrologium Romanum (1961) under Die 18 Decembris: Quintodecimo Kalendas Januarii: "Turonis, in Gallia, Sancti Gatiani Episcopi, qui, a Sancto Fabiano Papa primus ejusdem civitatis Episcopus ordinatus est, et multis clarus miracolis obdormivit in Domino".
  6. Fabian was highly esteemed by Cyprian. Cyprian's letter to Fabian's successor, Cornelius, calls him "incomparable" and says that the glory of his martyrdom answered the purity and holiness of his life (Cyprian, Epistle 30).
  7.  "Pope St. Fabian". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. 1913.
  8. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Fabian kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.