Sinodi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Sinodi (kwa Kiingereza "synod", kutoka maneno ya Kigiriki σύν, syun, "pamoja" na όδος, odos, "njia" = syunodos, yaani kufuata "njia ya pamoja", kwa hiyo "mkusanyiko" au "mkutano") ni mkutano wa Kanisa la Kikristo ambao huunganisha wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za Kanisa au eneo maalumu ndani ya Kanisa kama sinodi.

Kiasili sinodi ilikuwa mkutano wa maaskofu wa eneo fulani.

Wakati mwingine neno "mtaguso" hutumiwa kwa kutaja sinodi ya maaskofu wote, kwa mfano mtaguso mkuu ni mkutano wa maaskofu wote wa Kanisa Katoliki duniani.

Mara nyingi mkutano mkuu wa dayosisi au wa jimbo la Kanisa huitwa pia "sinodi".

Katika madhehebu ya Kiprotestanti sinodi hujumlisha wachungaji pamoja na walei.

Wapresbiteri hutumia neno "sinodi" kwa ajili ya mikoa yao ikitawaliwa na sinodi, yaani mkutano wa wajumbe kutoka shirika mbalimbali.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sinodi kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.