Jumuiya ya Afrika Mashariki
| Kaulimbiu: "One People, One Destiny" (Watu Mmoja, Hatima Moja) | |
| Wimbo wa taifa: "Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki" | |
| Mji mkuu | Arusha, Tanzania |
| Mji mkubwa | Kinshasa, Kongo JK |
| Lugha rasmi | Kiingereza |
| Lugha ya taifa | Kifaransa, Kiswahili |
| Serikali | Jumuiya ya Kikanda |
• Mwenyekiti wa Kikao cha Wakuu wa Nchi | William Ruto |
• Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri | Deng Dau Deng |
• Rais wa Mahakama ya EAC | Nestor Kayobera |
• Spika wa Bunge la Afrika Mashariki | Joseph Ntakarutimana |
• Katibu Mkuu | Veronica Nduva |
Historia | |
• Ilianzishwa | 1967 |
• Ilisambaratika | 1977 |
• Ilifufuliwa | 7 Julai 2000 |
| Eneo | |
| • Jumla | km2 5,449,717 km² |
| • Maji (asilimia) | 3.83% |
| Idadi ya watu | |
| • Kadirio la 2024 | ▲ 343,328,958 |
| • Msongamano | 63/km2 |
| PLT (PPP) | Kadirio la 2024 |
| • Jumla | ▲ $1.334 Trilioni |
| • Kwa kila mtu | ▲ $3,892 |
| PLT (Kawaida) | Kadirio la 2024 |
| • Jumla | ▲ $484.65 bilioni |
| • Kwa kila mtu | ▲ $1,438 |
| HDI (2022) | 0.515 chini |
| Sarafu | Sarafu mbalimbali (Shilingi ya Kenya, Shilingi ya Tanzania, Shilingi ya Uganda, Faranga ya Rwanda, Faranga ya Burundi, Pauni ya Sudan Kusini, Faranga ya Kongo) |
| Majira ya saa | UTC+3 EAT |
| Upande wa magari | Kushoto/Kulia (Inategemea Nchi) |
| Tovuti rasmi: www.eac.int | |
Jumuiya ya Afrika Mashariki (kifupi cha Kiingereza: EAC) ni shirika la kisiasa kati ya nchi nane za kanda ya Maziwa Makuu ya Afrika: Burundi, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda, Somalia, Sudan Kusini, Tanzania, na Uganda. Lengo kuu la EAC ni kukuza ushirikiano wa kikanda katika nyanja mbalimbali ikiwemo biashara, forodha, na ushirikiano wa kisiasa. Jumuiya hii ilianzishwa awali mwaka 1967, lakini ilisambaratika mwaka 1977 kutokana na tofauti za kisiasa, kabla ya kufufuliwa rasmi mwaka 2000 kwa kutiwa saini kwa mkataba mpya. Kwa sasa eneo la Mtangamano ni km2 4,810,363, likiwa na wakazi 312,362,653 (kadirio la mwaka 2022), hivi kwamba ingekuwa nchi moja tu ingekuwa ya nne duniani. Kuanzia mwaka 2024, William Ruto, Rais wa Kenya, ndiye mwenyekiti wake.
Tangu kufufuliwa kwake, Jumuiya ya Afrika Mashariki imeanzisha hatua mbalimbali muhimu za ujumuishaji, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa Umoja wa Forodha mwaka 2005, Soko la Pamoja mwaka 2010, na juhudi zinazoendelea kuelekea Muungano wa Fedha na hatimaye Shirikisho la Kisiasa. EAC pia imekuwa ikifanya kazi ya kuoanisha sera katika sekta kama usafiri, afya, elimu, na nishati. Ikiwa na jumla ya watu wanaozidi milioni 300 na msisitizo wa pamoja juu ya maendeleo ya kikanda, EAC ina nafasi inayoongezeka katika masuala ya bara na inachukuliwa kama mfano wa ushirikiano wa kikanda barani Afrika.[1][2][3][4]
Jumuiya ya Afrika Mashariki inaendesha shughuli zake kupitia taasisi kuu kadhaa zilizoanzishwa na mkataba wake wa kuanzishwa, zikiwemo Mkutano wa Wakuu wa Nchi au Serikali, Baraza la Mawaziri, Bunge la Afrika Mashariki, na Mahakama ya Afrika Mashariki, huku makao makuu yake yakipatikana Arusha, Tanzania; jumuiya hii hufanya kazi kwa kuzingatia itifaki na sheria zilizokubaliwa ambazo ni lazima kufuatwa na nchi wanachama, hasa katika maeneo kama udhibiti wa forodha, sera za biashara, na uhuru wa watu kusafiri, na Kiingereza ndiyo lugha rasmi zinazotumika, ambapo Kiswahili kimepitishwa mahsusi ili kuimarisha mawasiliano ya kikanda na ushirikiano.
Demografia
Idadi ya Watu
Jumuiya ya Afrika Mashariki ina idadi ya watu takriban milioni 333.93 ambapo aslimia 31 wanaishi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo , Sudan Kusini ndiyo iliyo na watu wachache sana ikiwa na watu takriban milioni 11.48 .Asilimia ya wakazi wanaoishi mijini ni 20 tu, lakini wanaongekeza kwa 4.71% kila mwaka
- Kongo JK 105.83 (31.7%)
- Tanzania 66.62 (19.9%)
- Kenya 55.53 (16.6%)
- Uganda 48.86 (14.6%)
- Somalia 18.36 (5.49%)
- Rwanda 13.95 (4.17%)
- 13.69 (4.09%)
- Sudan Kusini 11.48 (3.43%)
| Pangilio | Nchi | Idadi ya Watu (milioni) | Asilimia |
|---|---|---|---|
| 1 | 105.83 | 31.69 | |
| 2 | 66.62 | 19.95 | |
| 3 | 55.34 | 16.57 | |
| 4 | 48.66 | 14.57 | |
| 5 | 18.36 | 5.50 | |
| 6 | 13.95 | 4.18 | |
| 7 | 13.69 | 4.10 | |
| 8 | 11.48 | 3.44 |
Dini
Ukristo ndiyo dini kubwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa na wafuasi milioni 261.86 na asilimia 79% ya watu wa EAC, Kongo,JK ndio iliyo na wafuasi wengi takriban milioni 100 au asilimia 95.4 . Uislamu ina wafuasi takriban milioni 56.69 ambayo ni asilimia 16.98 ya watu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiongozwa na Somalia ambapo 99 ni waislamu. Dini za jadi ni asilimia 2.4% haswaa Sudan Kusini ambapo asilimia 35 ni wafuasi wa dini za jadi, Wasio na dini ni asilimia 1.75%
- Ukristo 261.86 (78.4%)
- Uislamu 56.69 (17.0%)
- Dini za Jadi 8 (2.40%)
- Wasio na Dini 5.83 (1.75%)
- Zingine 1.53 (0.46%)
| Pangilio | Nchi | Ukristo (%) | Uislamu (%) | Dini za Jadi (%) | Wasio na Dini (%) |
|---|---|---|---|---|---|
| 1 | 85.9 | 4.3 | 2.1 | 6.2 | |
| 2 | 85.5 | 10.9 | 0.7 | 1.5 | |
| 3 | 95.4 | 1.5 | 2.6 | 2.5 | |
| 4 | 93.8 | 2.2 | – | 3.0 | |
| 5 | – | 99.8 | – | – | |
| 6 | 60.5 | 6.2 | 32.9 | – | |
| 7 | 63.1 | 34.1 | 1.2 | 1.5 | |
| 8 | 81.7 | 13.2 | – | 0.2 |
Lugha
Kiswahili, Kiingereza na Kifaransa ndizo Lugha rasmi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika kama Lingua Franca katika nchi hizi huku Kiingereza na Kifaransa zikitumika kama lugha za kufundishia shuleni. Lugha za Jumuiya ya Afrika mashariki zimegawanyika katika kundi tatu ambazo ni Lugha za Kibantu ambayo ndiyo kundi kubwa ya Lugha katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Lugha za Kinilotiki na Lugha za Kikushi.
Mijini na Vijijini
Asilimia ya watu walioishi mijini katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni 35% na walioishi Vijijini asilimia 64%. Somalia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ndizo nchi zilizokuwa na asilimia kubwa ya wakazi wa mijini zikiwa na asilimia 46% na 45% mtawaliwa. Burundi na Sudan Kusini ndizo nchi zilizokuwa na wakazi wa mjini wachache sana zikiwa na asilimia 13% na 17% ya wakazi wanaoishi mijini huku asilimia 86% na 82% mtawaliwa wakiishi vijijini.
| Rank | Nchi | Mijini (%) | Vijijini (%) | Wakazi (Mijini) (milioni) |
|---|---|---|---|---|
| – | Jumuiya ya Afrika Mashariki | 35.13 | 64.87 | 117.30 |
| 1 | 46.73 | 53.27 | 8.58 | |
| 2 | 45.64 | 54.36 | 48.30 | |
| 3 | 37.41 | 62.59 | 24.92 | |
| 4 | 28.49 | 71.51 | 15.77 | |
| 5 | 26.77 | 73.23 | 13.03 | |
| 6 | 20.85 | 79.15 | 2.39 | |
| 7 | 17.72 | 82.28 | 2.47 | |
| 8 | 13.40 | 86.60 | 1.83 |
Muhtasari
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), yenye makao yake makuu Arusha, Tanzania,kazi yake kuu ni kuendeleza muungano wa kiuchumi, kisiasa, na kijamii katika ukanda huu. Mwenyekiti wa sasa wa EAC ni William Ruto, Rais wa Kenya, anayeongoza Mkutano wa Wakuu wa Nchi, ambao ndio chombo cha juu zaidi cha maamuzi katika jumuiya hii.
Kwa miaka iliyopita, EAC imepiga hatua muhimu ikiwemo kuanzishwa kwa Umoja wa Forodha, Soko la Pamoja, na mikataba ya kuunda Umoja wa Fedha. Pia imeongeza uanachama wake, ikiwemo kuipokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ,Somalia na Sudan Kusini. Miradi mikubwa ya miundombinu ya kikanda, programu za kurahisisha biashara, na ushirikiano katika sekta za afya na usalama ni miongoni mwa mafanikio yanayoonyesha ushawishi unaokua wa jumuiya hii katika kuendesha mipango ya maendeleo ya Afrika Mashariki.
Historia
Jumuiya ya kwanza
Nchi tatu za Afrika ya Mashariki zilizokuwa chini ya utawala wa Uingereza zilianza uhuru wao kwa kuendeleza ushirikiano wa karibu uliorithiwa kutokana na utawala wa pamoja wakati wa ukoloni.
Baada ya kupata uhuru mwaka 1961 nchi hizo ziliunda Mamlaka ya Huduma za Pamoja za Afrika ya Mashariki (kwa Kiingereza East African Common Services Organisation – kifupi EACSO).
Ushirikiano ulihusu fedha (East African Shilling), forodha (Customs Union), huduma za reli (East African Railway), ndege (East African Airways), mabandari, posta na simu na elimu ya juu (Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki chenye kampasi Makerere, Dar es Salaam na Nairobi). Mkataba ulilenga pia mahakama kuu ya pamoja na sera ya kiuchumi ya soko la pamoja. Haya yote yalitakiwa kuwa chini ya Bunge la Afrika Mashariki.
Tangu 1965 umoja huo ulianza kurudi nyuma kila nchi ilipoanzisha pesa yake.
Mwaka 1967 nchi tatu zilijaribu upya kuimarisha umoja wao kwa Mkataba wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki wakiita umoja wao "Jumuiya ya Afrika ya Mashariki" ikiwa na makao makuu Arusha, Tanzania.
Lakini mielekeo ya nchi zote tatu zilitofautiana mno: Kenya iliendelea kwa njia ya upebari lakini Tanzania ilijaribu kujenga Ujamaa (usoshalisti) kuanzia mwaka 1967. Uganda uliingia katika kipindi cha udikteta kali ya Idi Amini aliyeharibu uhusiano na majirani alipoanza kudai sehemu za maeneo yao.
Sababu nyingine ni madai ya Kenya ya kuwa na viti zaidi kuliko Uganda na Tanzania katika kamati za maamuzi,[5] huku kukiwa na kutokuelewana kulikosababishwa na udikteta wa Idi Amin nchini Uganda, Usoshalisti huko Tanzania, na soko huria nchini Kenya,[2] hivyo wanachama hawa watatu wakapoteza ushirikiano wa miaka zaidi ya sitini na manufaa ya ukubwa wa jumuiya hii kiuchumi. Kila mmoja wa wanachama hawa ilimbidi kuanza kutoa huduma na kujenga viwanda ambavyo hapo awali vilikuwa chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Hivyo mwaka 1977 Jumuiya ya Afrika Mashariki ilikoma kufanya kazi yoyote na 1983 ilifutwa rasmi. Mali iliyobaki iligawanywa kati ya nchi zote tatu.
Kufufuka kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki tangu 1993
Tangu miaka ya 1990 majaribio ya kujenga umoja mpya yalionekana tena.
Marais Daniel arap Moi wa Kenya, Ali Hassan Mwinyi wa Tanzania, na Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda walipatana katika Mkataba wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki huko Arusha, tarehe 30 Novemba 1993, na kuanzisha Tume ya Ushirikiano ya nchi hizi tatu. Shughuli ya kuzileta pamoja nchi hizi kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni, utafiti na teknolojia, ulinzi, usalama, masuala ya kisheria na kimahakama ilianza.
Mkataba wa kufufua jumuiya ulitiwa sahihi tarehe 30 Novemba 1999 ukaanza kuwa rasmi tarehe 7 Julai 2000.
Vyombo vya Jumuiya mpya ya Afrika ya Mashariki vilianza kufanya kazi mnamo Januari 2001 penye makao makuu ya jumuiya hii huko Arusha.
Mkataba 2004 uliweka msingi wa Umoja wa Forodha ulioanzishwa 2005.
Kuna tena Bunge la Afrika ya Mashariki linalojumuisha wabunge waliochaguliwa na mabunge ya nchi wanachama.
Pia Mahakama Kuu ya Afrika ya Mashariki imeundwa upya.
Mwaka 2008, baada ya majadiliano na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community, kifupi SADC) na Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (Common Market for Eastern and Southern Africa, kifupi COMESA), Mtangamano huo ulikubali nchi zote za miundo hiyo mitatu ziunde eneo pana la biashara huria. Kwa sasa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mojawapo ya nguzo muhimu za hiyo Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika (African Economic Community, kifupi AEC).
Mwaka 2010, Mtangamano ulitangaza soko la pamoja kwa bidhaa, kazi na mitaji kati ya nchi hizo tano, kwa lengo la kuanzisha pesa ya pamoja na hatimaye Shirikisho kamili.[6]
Kuna majadiliano ya kuanzisha shilingi mpya ya pamoja kwa nchi za Jumuia ya Afrika ya Mashariki. Kwanza ilitarajiwa kuanzishwa mwaka 2012, halafu mwaka 2015, sasa mwaka 2024. Mwaka 2013 ulisainiwa mkataba wa kuamua kuanzisha hiyo pesa ndani ya miaka 10.[7]
Uchumi
Uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unawakilisha mojawapo ya kanda zenye ukuaji wa haraka zaidi katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, ukichochewa na uimarishaji wa ushirikiano wa kikanda, uongezeko wa idadi ya watu, na uwekezaji wa kimkakati katika miundombinu. Jumla ya Pato la Taifa la Jumuiya, ilifikia takriban dola za Marekani bilioni 441.43 kufikia mwaka 2022, huku Pato la taifa kwa usawa wa nguvu ya ununuzi likifikia dola Trilioni 1.274. [8] Kanda ilirekodi wastani wa ukuaji wa asilimia 5.5 mwaka 2024 [9], ukipita wastani wa kimataifa wa asilimia 3.3 na wastani wa Kusini kwa Sahara wa asilimia 4.0, huku makadirio ya 2025 yakionyesha kuongeza kasi hadi asilimia 5.8. [10] Nchi zenye ukuaji wa juu zaidi ni pamoja na Rwanda ikiwa na asilimia 7.0, Tanzania asilimia 6.1, Burundi asilimia 6.0, na Uganda asilimia 5.9, huku Somalia ikitarajiwa kukua kwa wastani wa asilimia 3.5 hadi 4.0 kutokana na mageuzi ya kiuchumi yanayoendelea na usaidizi wa kimataifa. [11] Ingawa kanda inakabiliwa na changamoto endelevu zikiwemo viwango tofauti vya mfumuko wa bei na udhaifu wa kifedha, jumla ya biashara ya nje ilifikia dola za Marekani bilioni 130 mwaka 2024, huku sekta za huduma na teknolojia zikiendelea na mageuzi yake ya haraka. [12]
Sekta
Kilimo

Kilimo kinajumuisha sekta ya msingi ya uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kikichangia takriban asilimia 30 ya Pato la Taifa la kanda na kuajiri inakadiriwa asilimia 60 ya wakazi. [13] Sekta hii ina sifa ya ukulima mdogo wa mazao muhimu ya kuuza nje, yakiwemo kahawa, chai, maua bustani, mazao ya kilimo cha bustani, na viungo. Nchini Somalia, ufugaji wa mifugo unachangia takriban asilimia 40 ya Pato la Taifa na asilimia 50 ya mapato ya mauzo ya nje, huku wanyama hai wakisafirishwa hasa kuelekea masoko ya Ghuba ya Uajemi. [14] Kanda kwa ujumla ina nafasi muhimu kimataifa katika uzalishaji na usafirishaji wa mazao haya ya biashara, ingawa ongezeko la thamani ndani ya Jumuiya bado ni finyu ikilinganishwa na uwezo uliopo.
Licha ya umuhimu wake, sekta ya kilimo inaonyesha pengo endelevu la uwekezaji. Matumizi ya umma katika kilimo katika nchi kadhaa wanachama yanasalia chini ya lengo la asilimia 10 lililowekwa na Azimio la Malabo na Azimio la Kampala la Mpango Kamilifu wa Maendeleo ya Kilimo Afrika la mwaka 2025. [15] Mgao wa sasa katika nchi kubwa kama vile Kenya unakadiriwa kuwa asilimia tatu ya bajeti ya taifa, kiwango kinachozuia uboreshaji wa tija na maendeleo ya miundombinu ya vijijini. [16] Kutimiza malengo yaliyowekwa ya uwekezaji kunaweza kuongeza tija ya kilimo kwa wastani wa asilimia 45 na kupunguza kwa kiasi kikubwa upotevu wa mazao baada ya kuvuna.
Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki imeweka kipaumbele katika uboreshaji wa kisasa wa kilimo kuelekea mifumo inayostahimili mabadiliko ya hali ya hewa na inayoongozwa na thamani. Mipango inayoendelea inalenga kuboresha miundombinu ya vijijini, kupanua upatikanaji wa teknolojia na utafiti wa kilimo, kuimarisha ujumuishwaji wa kifedha kwa wakulima wadogo, na kukuza mbinu endelevu za usimamizi wa ardhi. [17] Sekta hii inakabiliwa na shinikizo linaloongezeka kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, yakiwemo ukame wa mara kwa mara na mafuriko, hali inayohitaji hatua za haraka za kukabiliana. Katika Pembe ya Afrika, ukame wa mara kwa mara umeathiri vibaya ufugaji wa mifugo nchini Somalia, na kusababisha juhudi za kikanda za kujenga uthabiti kupitia mipango ya bima ya mifugo na uboreshaji wa malisho. [14]
Viwanda na Uzalishaji
Sekta ya viwanda ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki iko katika awamu ya maendeleo, huku uzalishaji ukichangia sehemu ndogo lakini inayoongezeka ya Pato la Taifa katika nchi nyingi wanachama. Shughuli za kiviwanda zimejikita zaidi katika usindikaji wa mazao ya kilimo, vifaa vya ujenzi, uzalishaji mdogo wa bidhaa, na uchimbaji wa rasilimali za madini. [18] Mkakati wa maendeleo ya kitaifa wa Tanzania unatoa kipaumbele kwa uzalishaji kama kichocheo cha mageuzi ya kiuchumi, huku Uganda ikitarajia mabadiliko ya kimuundo kwa kuanza kwa uzalishaji wa mafuta ghafi katika mwaka wa fedha wa 2025/2026, maendeleo yanayotarajiwa kuinua kwa kiasi kikubwa ukuaji wa Pato la taifa. [19]
Bidhaa za madini zinajumuisha sehemu muhimu ya mfuko wa mauzo ya nje wa kanda. Mauzo ya nje yamejikita katika shaba, madini ya thamani na mawe, na mafuta ya madini. Sekta inayoibuka ya mafuta nchini Uganda inaungwa mkono na uwekezaji wa kipaumbele katika miundombinu, ikiwemo ujenzi wa bomba la mafuta kwa ajili ya usafirishaji wa mafuta ghafi. [20] Kujiunga kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki kumepanua kwa kiasi kikubwa utajiri wa madini wa kanda hiyo, hasa katika madini ya kobalti, shaba, na koltan. [21] Nchini Somalia, sekta ya viwanda bado ni changa, ikijikita katika usindikaji wa mazao ya wanyama kama vile ngozi na mifugo, pamoja na uzalishaji mdogo wa bidhaa za matumizi ya ndani na uvuvi wa kibiashara katika ukanda wake mrefu wa pwani. [14]
Utalii

Utalii unachangia chanzo muhimu cha fedha za kigeni na ajira kwa nchi several wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hasa Kenya, Tanzania ikijumuisha funguvisiwa la Zanzibar lenye kujitawala, Rwanda, na Uganda. [22] Sekta hii imeonyesha ahueni thabiti baada ya janga la ugonjwa, ikichochewa na rasilimali za kipekee za wanyamapori za kanda, vivutio vya pwani, na urithi wa kitamaduni. Somalia ina uwezo mkubwa wa kitalii ambao bado haujatumika kikamilifu, ikiwemo fuo zake refu zaidi barani Afrika, visiwa visivyo na watu, na maeneo ya kihistoria ya miji ya kale ya pwani, ingawa ukosefu wa usalama na miundombinu duni vimezuia maendeleo makubwa ya sekta hii.
Zanzibar ni mfano wa mwelekeo wa ukuaji wa sekta hii. Mwaka 2025, watalii wa kimataifa waliowasili walikaribia milioni moja, wakionyesha ongezeko la asilimia 7.1 ikilinganishwa na mwaka uliopita, huku mapato ya utalii yakizidi dola za Marekani bilioni 1.1, zote zikiwa rekodi za juu. [23] Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar imesajili zaidi ya miradi 1,300 ya uwekezaji yenye thamani ya jumla ya dola za Marekani bilioni 14.3, huku utalii ukichangia zaidi ya asilimia 50 ya mfumo huu wa uwekezaji. [24] Eneo hili linapitia mabadiliko ya kimkakati kutoka kwa mfumo wa jadi wa utalii wa pwani kuelekea mseto unaojumuisha Mikutano, Vivutio, Makongamano, na Maonyesho, usafiri wa ustawi, utalii wa upishi, na mipango ya wahamaji wa kidijitali.
Utalii wa kikanda uko tayari kwa upanuzi zaidi kwa kuandaa mashindano yajayo ya Kombe la Mataifa ya Afrika, ambapo Nchi Wanachama zinaandaa uboreshaji wa miundombinu ikijumuisha upanuzi vya vituo vya ndege na kuboresha mitandao ya barabara. [25] Bajeti za kitaifa katika Jumuiya nzima zinatilia mkazo kipaumbele utalii pamoja na sekta nyingine za ukuaji.
Biashara ya Kimataifa
Mnamo 2023, jumla ya biashara ya kimataifa ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ilifikia dola bilioni 130.4. [26] Mchango mkubwa zaidi ulitoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (JKK), ambayo ilichangia asilimia 25.8 ya jumla hiyo, ikifuatiwa na Kenya (24.7%) na Tanzania (24.6%). Kwa upande mwingine, nchi zilizo na mchango mdogo zaidi zilikuwa Sudan Kusini (1.8%) na Burundi (0.7%). Kwa Mahuruji (mauzo ya nje) Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo iliongoza zaidi ikichangia asilimia 40% ya mauzo ya nje ya Jumuiya hii, Huku Kenya ikiongoza kwa Maduhuli ikichangia asilimia 30% ya Maduhuli ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kati ya nchi zote, Kongo,JK ilikuwa na mizani chanya ya biashara (balance of trade) ya dola bilioni 7.8, ikiwa ya juu zaidi katika kanda, huku Kenya (-16.24), Tanzania (-9.90), na Somalia (-4.22) zikiripoti nakisi kubwa zaidi ya biashara, ishara ya uagizaji mkubwa wa bidhaa kuliko mauzo ya nje. [26]
| Rank | Nchi | Jumla | Mahuruji | Maduhuli | Mizani ya Biashara |
|---|---|---|---|---|---|
| 1 | 33.60 | 20.70 | 12.90 | 7.80 | |
| 2 | 32.16 | 7.96 | 24.20 | -16.24 | |
| 3 | 32.10 | 11.10 | 21.00 | -9.90 | |
| 4 | 19.69 | 8.39 | 11.30 | -2.91 | |
| 5 | 6.11 | 0.95 | 5.16 | -4.22 | |
| 6 | 3.55 | 1.35 | 2.20 | -0.85 | |
| 7 | 2.32 | 0.70 | 1.62 | -0.92 | |
| 8 | 0.87 | 0.20 | 0.68 | -0.48 | |
| 130.40 | 51.35 | 79.06 | -27.71 | ||
Pato la taifa
Jumuiya ya Afrika Mashariki ina uchumi unaoendelea ikiwa na Pato la taifa jumla dola bilioni 441.43 za Marekani kwa Kawaida na trilion 1.274 kwa Usawa wa nguvu ya ununuzi (PPP) hata hivyo ni uchumi wa pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya Afrika Kusini. [27] Kenya ndiyo iliyo na uchumi mkubwa zaidi katika jumuiya hii, ikichangia asilimia 31.91% ya jumla, Tanzania, Kongo, JK zilichangia asilimia 21.6% na 19.9% mtawaliwa. [28] Sudan kusini na Burundi ndizo zilizokuwa na uchumi mdogo zaidi. Jumuiya ya Afrika Mashariki ni ya kipato cha chini ikiwa na pato la taifa kwa kila mtu dola 1,274 . Sudan Kusini ndiyo nchi maskini zaidi ikiwa na pato la taifa kwa kila mtu dola 369 za Marekani, Kenya ndiyo nchi iliyo na pato la taifa kwa kila mtu dola kubwa zaidi ya dola 2,596 za Marekani. [27]
| Orodha | Nchi | PLT (Kawaida) 'bilioni USD | PLT (PPP) 'bilioni USD | Kwa kila mtu (Kawaida) | Kwa kila mtu (PPP) | Asilimia ya EAC |
|---|---|---|---|---|---|---|
| – | 484.65 | 1,334.52 | $1,413 | $3,892 | 100.0% | |
| 1 | 147.26 | 435.23 | $2,713 | $8,020 | 30.38% | |
| 2 | 123.41 | 235.94 | $1,122 | $2,145 | 25.46% | |
| 3 | 94.89 | 320.88 | $1,362 | $4,607 | 19.58% | |
| 4 | 73.37 | 208.38 | $1,476 | $4,192 | 15.14% | |
| 5 | 17.34 | 65.46 | $1,198 | $4,524 | 3.58% | |
| 6 | 14.17 | 34.11 | $812 | $1,956 | 2.92% | |
| 7 | 8.14 | 15.36 | $546 | $1,031 | 1.68% | |
| 8 | 6.07 | 19.16 | $488 | $1,540 | 1.25% |
| Orodha | Nchi | PLT (Kawaida) 'bilioni USD | PLT (PPP) 'bilioni USD | Kwa kila mtu (Kawaida) | Kwa kila mtu (PPP) | Asilimia ya EAC |
|---|---|---|---|---|---|---|
| – | 484.65 | 1,334.52 | $1,413 | $3,892 | 100.0% | |
| 1 | 147.26 | 435.23 | $2,713 | $8,020 | 30.38% | |
| 2 | 123.41 | 235.94 | $1,122 | $2,145 | 25.46% | |
| 3 | 94.89 | 320.88 | $1,362 | $4,607 | 19.58% | |
| 4 | 73.37 | 208.38 | $1,476 | $4,192 | 15.14% | |
| 5 | 17.34 | 65.46 | $1,198 | $4,524 | 3.58% | |
| 6 | 14.17 | 34.11 | $812 | $1,956 | 2.92% | |
| 7 | 8.14 | 15.36 | $546 | $1,031 | 1.68% | |
| 8 | 6.07 | 19.16 | $488 | $1,540 | 1.25% |
Nchi Wanachama


| Nchi | Mji mkuu | Kujiunga | Wakazi | Eneo (km2) | GDP (US$ bn)[29] |
GDP kwa mtu (US$)[29] |
GDP PPP (US$ bn)[30] |
GDP PPP kwa mtu (US$)[30] |
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Gitega | 2007 | 12,722,976 | 27,834 | 3.4 | 272.4 | 10.8 | 855.6 | |
| Kinshasa | 2022 | 95,944,984 | 2,344,858 | 51.2 | 669.4 | 127.4 | 1,315.9 | |
| Nairobi | 2000 | 56,553,921 | 580,367 | 114.7 | 2,252 | 308.7 | 6,061.4 | |
| Kigali | 2007 | 13,705,697 | 26,338 | 12.1 | 910 | 37.2 | 2,807.6 | |
| Mogadishu | 2024 | 16,500,000 | 637,657 | 12.49 | 756.98 | 34.02 | 2,060 | |
| Juba | 2016 | 11,501,583 | 644,329 | 5.7 | 392.7 | 13.5 | 927.4 | |
| Dodoma | 2000 | 63,732,235 | 945,087 | 77.5 | 1,260.1 | 206.6 | 3,358.3 | |
| Kampala | 2000 | 49,135,753 | 241,550 | 46.4 | 1,060.4 | 129.5 | 2,960.5 | |
| 303,397,152 | 4,810,363 | 325 | 1106.3 | 834 | 2,841.4 | |||
Kenya, Tanzania na Uganda zina historia ya ushirikiano tangu mwanzoni mwa karne ya 20, wakati wa ukoloni, ikiwa ni pamoja na Umoja wa Forodha baina ya Kenya na Uganda mwaka 1917, Tanganyika ilijiunga mnamo mwaka 1927, katika Ubalozi wa Afrika Mashariki (1948-1961), 'East African Common Services Organisation' (1961-1967) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (1967-1977).[31]
Jumuia ambayo ilianzishwa baada ya uhuru ilidumu miaka 10 tu, lakini ilifufuliwa kwa mkataba wa tarehe 30 Novemba 1999, ulioanza kufanya kazi tarehe 7 Julai 2000, miaka 23 baada ya kifo cha ile ya kwanza.
Burundi na Rwanda, ambazo ziliwahi kuwa koloni moja na Tanzania bara kabla ya Vita vikuu vya kwanza, zilijiunga na Mtangamano tarehe 6 Julai 2009.[32]
Mara baada ya kupata uhuru mwaka 2011, Sudan Kusini iliomba kujiunga na Jumuia, lakini haikukubalika hadi Machi 2016 kutokana na hali ya vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Tarehe 23 Novemba 2021 Baraza la Mawaziri la EAC limependekeza kwa Wakuu wa nchi wanachama wakubali ombi la kujiunga la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo [33], nao wakakubali rasmi tarehe 29 Machi 2022.
Hatua kubwa ya awali katika kuanzisha Shirikisho la Afrika Mashariki ni muungano wa forodha katika mataifa husika uliotiwa saini mnamo Machi 2004 na ulioanza kutumika tarehe 1 Januari mwaka 2005. Chini ya masharti ya mkataba, Kenya, ambayo ndiyo nchi inayopata mauzo bora zaidi nje ya nchi katika kanda ya Afrika Mashariki, iliendelea kulipa ushuru kwa bidhaa zake zinazoingia nchi nyingine wanachama hadi mwaka 2010, kwa kiwango kilichopungua na wakati. Mfumo sawa wa ushuru utatumika kwa bidhaa kutoka nchi ambazo si wanachama.
Changamoto
Kwa ujumla, mataifa wanachama kwa kiasi kikubwa wanaona neema ya Shirikisho la Afrika Mashariki, lakini utafiti usio rasmi unaonyesha kwamba Watanzania wengi (asilimia themanini ya wakazi wake) wana mtazamo hasi.[34]
Tanzania imekuwa na historia ya amani tangu kunyakua uhuru, ikilinganishwa na fujo na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoshuhudiwa katika mataifa ya Kenya, Rwanda, Burundi, na Uganda. Wakati huu Afrika Mashariki inajaribu kudumisha utulivu na mafanikio katikati ya migogoro inayoendelea katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Pembe ya Afrika na Sudan Kusini.
Pia ni kwamba Tanzania ina ardhi kubwa, na baadhi ya Watanzania wana hofu ya unyakuzi wa ardhi na wakazi wa sasa wa mataifa mengine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.[35] [36] [37]
Uhaba wa ardhi ni suala nyeti katika eneo la Afrika Mashariki, hasa nchini Kenya, ambako mapigano ya wenyewe kwa wenyewe upande wa Mlima Elgon mwaka 2007 yaliwaacha zaidi ya watu 150 wamefariki na kulazimisha takriban watu wengine 60,000 kugura makazi yao.[38]
Serikali na Utawala
Mahakama ya Afrika Mashariki
Mahakama ya Afrika Mashariki ndiyo mahakama inayosimamia kesi zote katika eneo hilo. Kwa sasa imo mjini Arusha, Tanzania.
Bunge la Afrika Mashariki

Bunge la Afrika Mashariki ndicho kitengo cha kutengeneza sheria katika eneo la Afrika Mashariki. Ina wajumbe 27 ambao wote wamechaguliwa na mabunge ya nchi wanachama. Linahusika na masuala yote ambayo yanahusu Jumuiya hii kama vile kujadili bajeti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na masuala yote ya Jumuiya na kutoa mapendekezo kwa Baraza juu ya mambo wanayoyadhani muhimu kwa utekelezaji wa mkataba, kushirikiana pamoja na Bunge husika na kuanzisha kamati kwa makusudi kama vile wanavyodhani ni muhimu. Tangu uzinduzi wake mwaka 2001, bodi hii imekuwa na vikao kadhaa mjini Arusha, Kampala na Nairobi.
Viungo
Pasipoti ya Afrika Mashariki
Pasipoti ya Afrika Mashariki ilizinduliwa rasmi tarehe 1 Aprili 1999 ili kurahisisha usafiri na kuvuka mipaka ya nchi husika.[39][40] Ni halali kwa kusafiri ndani ya eneo la Afrika Mashariki (Kenya,Uganda na Tanzania) na kutoa haki ya kuingia na kukaa kwa miezi sita katika nchi yoyote na kisha unaweza ukaitumia tena.[39] Pasipoti hii inapatikana katika Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji katika miji ya Nairobi, Kampala na Dar es Salaam. Ni raia tu wa Afrika Mashariki wanaoweza kuomba pasipoti hii.[39][40] Gharama ya pasipoti hii ni dola 10 za Marekani au pesa sawa ukibadilisha kwa sarafu za nchi za Afrika mashariki.[40] Baada ya kujaza fomu za kupata pasipoti hii itachukua muda wa wiki mbili au tatu kuipata tayari kwa matumizi. Ingawa pasipoti hii ni halali tu ndani ya Afrika Mashariki, majadiliano yalifanywa ili kuwa na hati sawa za kusafiri kwa watu wote wa Afrika Mashariki.[39]
Viza moja kwa watalii
| African Union |
Makala hii imepangwa kwa mfululizo: |
|
|
|
Executive
Legislature
Judiciary
Advisory bodies
Financial bodies
Decentralised bodies
|
|
Nchi zingine · Atlasi |
Lilikuwa tarajio la wengi kuwa kabla ya 2006 kungekuwa na viza moja kwa watalii wote wanaozuru Afrika Mashariki, iwapo mpango huo ungeidhinishwa na mamlaka ya sekta husika chini ya jumuiya hiyo. Iwapo ingekubalika basi viza hiy ingetumika kote katika ardhi ya wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Chini ya pendekezo hili viza yoyote mpya ya Afrika Mashariki ingeweza kupokewa kutoka ubalozi wowote katika eneo la Afrika Mashariki.
Mtandao
Matumizi ya wavuti katika eneo la Afrika Mashariki bado yako chini mno yakilinganishwa na mataifa yaliyostawi kiuchumi.
Eneo la Afrika Mashariki ni kituo kizuri kiuchumi huku likikadiriwa kuwa na wakazi zaidi ya milioni 150. Inakadiriwa kuwa asilimia 10 ya wakazi wa Afrika Mashariki - milioni 15 - huutumia Mtandao.
Mkakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unasisitiza ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo kwa kuzingatia uwezo wa kijamii.
Wengi wa wakazi wa Afrika Mashariki hutumia mtandao kuangalia habari, kusoma barua pepe na kwenye mitandao mingine ya kijamii.
Hivi karibuni kumekuwa na majukwaa mengi yanayoibuka katika eneo hili kwa lengo la kuileta pamoja Afrika Mashariki.
Kasi ya mawasiliano kupitia kwa mtandao pia iko chini mno katika eneo la Afrika Mashariki, ikilinganishwa na mataifa yaliyostawi. Hii labda ni mojawapo ya vikwazo vya maendeleo ya mawasiliano ya mtandao Afrika Mashariki.
Jiografia
Mtangamano ungekuwa nchi moja tu, ungekuwa ya 7 duniani kwa eneo (kilometa mraba 4,812,618).
Sudan Kusini, Uganda, Rwanda na Burundi hazina pwani baharini, lakini zina mvua za kutosha.
Huku inapatikana minne kati ya milima mirefu zaidi barani Afrika: Mlima Kilimanjaro (Tanzania), Mlima Kenya (Kenya), milima ya Rwenzori (Uganda/DRC) na Mlima Meru (Tanzania).
Ziwa Turkana, Kenya, ndiyo ziwa la jangwani kubwa na lenye maji ya chumvi nyingi kuliko yote duniani.
Ziwa Victoria linaunganisha nchi za Kenya, Uganda na Tanzania na ni la pili duniani kwa eneo.
Ziwa Tanganyika kati ya Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni la pili duniani kwa kina.
Kenya pekee ina jangwa, jangwa la Chalbi katika Kaunti ya Marsabit.
Ugatuzi katika nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki (E.A.C.)
Burundi
Kenya
- Mombasa
- Kwale
- Kilifi
- Tana River
- Lamu
- Taita–Taveta
- Garissa
- Wajir
- Mandera
- Marsabit
- Isiolo
- Meru
- Tharaka-Nithi
- Embu
- Kitui
- Machakos
- Makueni
- Nyandarua
- Nyeri
- Kirinyaga
- Murang'a
- Kiambu
- Turkana
- West Pokot
- Samburu
- Trans-Nzoia
- Uasin Gishu
- Elgeyo-Marakwet
- Nandi
- Baringo
- Laikipia
- Nakuru
- Narok
- Kajiado
- Kericho
- Bomet
- Kakamega
- Vihiga
- Bungoma
- Busia
- Siaya
- Kisumu
- Homa Bay
- Migori
- Kisii
- Nyamira
- Nairobi
Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia
- Mkoa wa Équateur
- Mkoa wa Ituri
- Mkoa wa Kasai
- Mkoa wa Kasai Kati
- Mkoa wa Kasai Mashariki
- Mkoa wa Katanga Juu
- Mkoa wa Kinshasa
- Mkoa wa Kivu Kaskazini
- Mkoa wa Kivu Kusini
- Mkoa wa Kongo Kati
- Mkoa wa Kwango
- Mkoa wa Kwilu
- Mkoa wa Lomami
- Mkoa wa Lomami Juu
- Mkoa wa Lualaba
- Mkoa wa Mai-Ndombe
- Mkoa wa Maniema
- Mkoa wa Mongala
- Mkoa wa Sankuru
- Mkoa wa Tanganyika
- Mkoa wa Tshopo
- Mkoa wa Tshuapa
- Mkoa wa Ubangi Kaskazini
- Mkoa wa Ubangi Kusini
- Mkoa wa Uele Chini
- Mkoa wa Uele Juu
Rwanda
Somalia
Sudan Kusini
Tanzania
Uganda
Tazama pia
- Orodha ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Pato la taifa
- Orodha ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Kiashiria cha Maendeleo ya Binadamu
- Orodha ya Maeneo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Kiashiria cha Maendeleo ya Binadamu
- Orodha ya nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki kulingana na Umri wa Kuishi
- Shirikisho la Afrika Mashariki
- Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
- Uchumi wa Afrika
- Mamlaka ya Maendeleo ya Kitaifa (IGAD)
- Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)
- Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA)
- Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika ya Kati (ECCAS)
- Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Tanzania
Marejeo
- ↑ "– Born in anonymity". Ms.dk. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2012-04-15. Iliwekwa mnamo 2010-07-01.
- 1 2 East African trade zone off to creaky start, Christian Science Monitor, 9 Machi 2006
- ↑ We Celebrated at EAC Collapse, Says Njonjo.
- ↑ "East African Community – Quick Facts". Eac.int. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2009-03-19. Iliwekwa mnamo 2010-07-01.
- ↑ "ms.dk - Born in anonymity". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2012-04-15. Iliwekwa mnamo 2009-12-03.
- ↑ "FACTBOX-East African common market begins". Reuters. 1 Julai 2010. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2012-01-18. Iliwekwa mnamo 1 Julai 2010.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "East African trade bloc approves monetary union deal". Reuters. 30 Novemba 2013. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-09-24. Iliwekwa mnamo 2015-01-23.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "GDP IN EAST AFRICA COMMUNITY". IMF.org. International Monetary Fund. Aprili 2026. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ Ingrid Peters (2024). "East Africa Reports Impressive 5.4% economic growth in 2024". African Leadership Magazine. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "East Africa Economic Outlook". afdb.org. African Development Bank. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - ↑ "Somalia and the IMF". IMF.org. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "EAC Trade Report". eac.int. East African Community. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "East African Community (EAC)". Britannica. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - 1 2 3 "Somalia Economic Update". worldbank.org. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Tracking progress on the Malabo Declaration" (PDF). fao.org. 2023. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "National Budget Statements". treasury.go.ke. The National Treasury of Kenya. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Agriculture and Food Security in the EAC". eac.int. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Industrialization Strategy". eac.int. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - ↑ "Uganda Economic Analysis". Coface. 2025. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - ↑ "Petroleum Authority of Uganda". pau.go.ug. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "DRC Economy". Britannica. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Global Tourism Data Dashboard". unwto.org. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Zanzibar Tourism Hits New Record". Daily News Tanzania. Januari 15, 2026. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - ↑ "Zanzibar Investment Promotion Authority". zipa.go.tz. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "EAC to leverage AFCON 2027". eac.int. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - 1 2 "EAC Trade Report 2023". eac.int. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - 1 2 "World Economic Outlook Database: April 2026". IMF.org. Aprili 14, 2026. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "East Africa Economic Outlook 2024". afdb.org. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - 1 2 "Report for Selected Countries and Subjects". www.imf.org.
- 1 2 "Report for Selected Countries and Subjects". www.imf.org.
- ↑ From Co-operation to Community (eac.int)
- ↑ "EAC Update E-newsletter". www.eac.int. Directorate of Corporate Communications and Public Affairs. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2012-04-26. Iliwekwa mnamo 10 Desemba 2011.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ https://www.eac.int/press-releases/2288-eac-council-of-ministers-green-light-report-on-drc-verification-mission-for-consideration-by-eac-heads-of-state
- ↑ allAfrica.com: Tanzania: Fast-Tracking Political Federation
- ↑ EAC federation fears justified? Ilihifadhiwa 27 Septemba 2007 kwenye Wayback Machine. Tanzania's Daily News On Saturday; 5 Mei 2007
- ↑ Kenya: Tears for Mt Elgon as Schools Re-Open
- ↑ Sabiny Demand Land as Karamajong Raid Reduce
- ↑ AlertNet Ilihifadhiwa 20 Juni 2010 kwenye Wayback Machine. Kenya land clashes kill 60, displace thousands
- 1 2 3 4 "EAC News ..." Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2004-12-21. Iliwekwa mnamo 2004-12-21.
- 1 2 3 "Travelling in East Africa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2004-07-01. Iliwekwa mnamo 2004-07-01.
Viungo vya nje
- Jumuiya ya Afrika Mashariki
- German and East African Community Cooperation Ilihifadhiwa 16 Septemba 2015 kwenye Wayback Machine.
- Agritrade Agricultural trade in East Africa Ilihifadhiwa 14 Februari 2014 kwenye Wayback Machine.
- Information from africadatabase.org Ilihifadhiwa 29 Juni 2006 kwenye Wayback Machine.
- Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Ulaya Ilihifadhiwa 24 Februari 2012 kwenye Wayback Machine.
- EAC Free Trade Agreement
- Makala za Afrika
- Habari za BBC kuhusu kuanzishwa kwa Umoja wa Forodha
- Bunge la pamoja la Afrika Mashariki
- Habari za Biashara kuhusu Jumuiya ya Afrika Mashariki
- Rwanda na Burundi kujiunga na Afrika Mashariki allAfrica.com, 17 Oktoba 2006

