Uchumi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Uchumi


Uchumi ni jumla ya shughuli zote za binadamu zinazolenga kutosheleza mahitaji yao. Ni hasa uzalishaji, usambazaji na utumiaji wa bidhaa pamoja na kutolewa kwa huduma kwa njia mbalimbali.

Uchumi mara nyingi hutazamwa kwenye ngazi za kijiji, eneo, taifa au dunia.

Sayansi ya Uchumi (kwa Kiingereza economics) ni tawi la elimu inayochunguza masharti ya uchumi kufaulu au kushindwa.

Sekta za uchumi[hariri | hariri chanzo]

Uchumi wa jadi katika nchi nyingi ulikuwa hasa kilimo cha kujikimu pamoja na biashara ya kubadilishana bidhaa kadhaa zenye thamani kubwa. Kwa mfano, tangu kale migodi ya Zimbabwe ilichimba dhahabu iliyopelekwa baadaye hadi Asia na kando ya Mediteranea.

Katika uchumi wa kisasa mara nyingi sekta tatu hutofautishwa:

  • Sekta ya tatu: biashara au usambazaji wa bidhaa hizi kwa wateja pamoja na kuwatolea huduma. Mifano ni maduka yanayouza bidhaa zilizotengenezwa viwandani. Mingine ni huduma kama benki, hoteli, sinema na usafiri.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]


Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uchumi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.