Kaunti ya Mandera
| Kaunti ya Mandera | |
|---|---|
| Kaunti | |
| Kaulimbiu: "" | |
Kaunti ya Mandera katika Kenya | |
| Coordinates: 3°25′00″N 40°40′00″E / 3.41667°N 40.6667°E | |
| Nchi | |
| Nambari | 9 |
| Ilianzishwa | Tarehe 4 Machi, 2013 |
| Ilitanguliwa na | Mkoa wa Kaskazini Mashariki |
| Mji mkuu | Mandera |
| Miji mingine | El Wak |
| Serikali | |
| Gavana | Ali Ibrahim Roba |
| Naibu wa Gavana | Arai Mohamed Ahmed |
| Seneta | Mohamed Maalim Mahamud |
| Mwakilishi wa wanawake | Amina Gedow Hassan |
| Bunge | Bunge la Kaunti ya Mandera |
| Wawakilishi Wadi | 30 |
| Maeneo bunge | 6 |
| Eneo | |
| Jumla | km2 25 939.8 (sq mi 10 015.4) |
| Idadi ya Watu | |
| Jumla | 867,457 |
| Msongamano | 33 /km² |
| Majira ya Saa | Saa za Afrika Mashariki (UTC+3) |
| Tovuti mandera.go.ke | |
Kaunti ya Mandera ni mojawapo ya Kaunti 47 za Kenya iliyopo kaskazini mashariki mwa nchi. Inapakana na Ethiopia upande wa kaskazini, Somalia upande wa mashariki, na Kaunti ya Wajir upande wa kusini-magharibi. Kulingana na sensa ya 2019 kaunti hii ilikuwa na wakaazi 867,457 ikiwa kaunti ya 24 kwa idadi ya watu na eneo la km2 25,939.8 na kuwa kaunti ya 6 kwa ukubwa wa ardhi.[1].Mji mkubwa na makao makuu ni mji wa Mandera. Inajulikana kwa misukosuko ya usalama na uhamiaji kutoka Somalia
Jiografia
[hariri | hariri chanzo]Kaunti hii ina mbuga ya pekee ya Kaskazini Mashariki ya Malka Mari na hifadhi ya kibinafsi ya Chacnabole. Ina vilima vinavyotandaa kutoka El Wak hadi Uhabeshi ingawa kiasi kikubwa cha ardhi yake ni nchi tambarare.
Kuna kanda mbili za ikolojia, kavu na nusu kavu. 95% ya kaunti ni nusu kavu na huwa na vichaka vyenye miiba katika sehemu za chini za vilima[2].
Utawala
[hariri | hariri chanzo]Kaunti ya Mandera imegawanywa katika maeneo yafuatayo[3]:
Demografia
[hariri | hariri chanzo]Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [4]
[hariri | hariri chanzo]- Mandera West 98,300
- Banisa 152,598
- Kutulo 72,394
- Lafey 83,457
- Mandera Central 157,220
- Mandera East 159,638
- Mandera North 143,850
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-29.
- ↑ "KENYA INTER AGENCY RAPID ASSESSMENT MANDERA COUNTY CONFLICT ASSESSMENT REPORT 19TH – 30TH JUNE 2014", Kenya Inter Agency Assessment, ilipatikana 13-04-2018
- ↑ "Kaunti ya Mandera Ilihifadhiwa 9 Aprili 2018 kwenye Wayback Machine.", Infotrak, ilipatikana 13-04-2018
- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-29.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- http://softkenya.com/county/mandera-county/ Ilihifadhiwa 4 Aprili 2011 kwenye Wayback Machine. Mandela County
- Map of the District
- http://www.reliefweb.int/rw/RWB.NSF/db900SID/VBOL-6UEDLF?OpenDocument
| Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kaunti ya Mandera kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |