Kaunti ya Meru

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kuhusu makao makuu, tazama Meru

Kaunti ya Meru
Kaunti
Bendera Nembo ya Serikali
Meru County in Kenya.svg
Kaunti ya Meru katika Kenya
Coordinates: 0°3′N 37°38′E / 0.050°N 37.633°E / 0.050; 37.633Coordinates: 0°3′N 37°38′E / 0.050°N 37.633°E / 0.050; 37.633
Nchi Kenya
Namba12
IlianzishwaTarehe 4 Machi, 2013
Ilitanguliwa naMkoa wa Mashariki
Makao MakuuMeru
Miji mingineMaua, Nkubu
GavanaKiraitu Murungi, EGH
Naibu wa GavanaTitus Ntuchiu Mutea
SenetaMithika Linturi
Mbunge Mwanamke(Bunge la Taifa)Kawira Mwangaza
Bunge la KauntiBunge la Kaunti ya Meru
Wawakilishi wa Bunge la Kaunti waliochaguliwa45
MahakamaMahakama ya Rufaa, Meru
Maeneo bunge/Kaunti ndogo9
Eneo7,006.3 km2 (2,705.1 sq mi)
Idadi ya watu1,545,714
Wiani wa idadi ya watu221
Kanda mudaSaa za Afrika Mashariki (UTC+3)
Tovutimeru.go.ke

Kaunti ya Meru ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.

Jina lake limetokana na Wameru ambao ndio jamii kubwa zaidi katika kaunti hii.

Sehemu kubwa ya Meru ina ardhi ya rutuba na mvua ya kutosha. Ni kaunti inayojulikana kwa ukuzaji wa miraa, kama zao la biashara. Hata hivyo, ukulima wa ndizi, mahindi, majani ya chai na maharagwe hufanywa[1].

Wakati wa sensa ya mwaka 2019 wakazi walikuwa 1,545,714 katika eneo la km2 7,006.3, msongamano ukiwa hivyo wa watu 221 kwa kilometa mraba[2]..

Makao makuu yako Meru.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Kilimo cha kiazi cha kizungu.

Kaunti ya Meru inapakana na Kaunti za Nyeri, Laikipia, Tharaka Nithi, Isiolo na Kitui.

Iko katika upande wa mashariki mwa Mlima Kenya. Sehemu ya Mbuga ya Kitaifa ya Mlima Kenya iko katika Meru.

Mvua yenye kufaa pamoja na udongo wa volkano huwezesha kilimo. Sehemu za Imenti zilizo karibu na Mlima Kenya huwa ni baridi kidogo na zenye vilima. Sehemu za Tigania hazina hali za kufaa kulima isipokuwa karibu na Vilima vya Nyambene, ambapo huwa baridi kidogo. Mbuga ya Kitaifa ya Meru iko katika sehemu za Igembe, kaskazini mashariki mwa kaunti[3].

Mito, k.v. Mto Kathita hutoka Mlima Kenya na Vilima vya Nyambene na hutiririsha maji yake ndani ya Mto Tana[4].

Meru ni sehemu ya kati ya uliokuwa Mkoa wa Mashariki nchini Kenya upande wa mashariki-kaskazini wa mlima Kenya.

Eneo la Meru lilijumlishwa hadi 1992 katika wilaya ya Meru iliyogawiwa baadaye kuwa wilaya zifuatazo:

Utawala[hariri | hariri chanzo]

Kaunti ya Meru imegawanywa katika maeneo bunge yafuatayo:

Eneo bunge Kata
Igembe Kusini Maua, Kegoi/Antubochiu, Athiru Gaiti, Akachiu, Kanuni
Igembe ya Kati Akirang’ondu, Athiru Ruujine, Igembe Mashariki Njia, Kangeta
Igembe Kaskazini Antuambui, Ntunene, Antubetwe Kiongo, Naathui, Amwathi
Tigania Magharibi Athwana, Akithi, Kianjai, Nkomo, Mbeu
Tigania Mashariki Thangatha, Mikinduri, Kiguchwa, Mithara, Karama
Imenti Kaskazini Imenti Manispaa, Ntima Mashariki, Ntima Magharibi, Nyaki Magharibi, Nyaki Mashariki
Buuri Timau, Kisima, Kiirua/Naari, Ruiri/Rwarera
Imenti ya Kati Mwanganthia, Abothuguchi ya Kati, Abothuguchi Magharibi, Kiagu, Kibirichia
Imenti Kusini Mitunguu, Igoji Mashariki, Igoji Magharibi, Abogeta Mashariki, Abogeta Magharibi, Nkuene

Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [5][hariri | hariri chanzo]

  • Buuri East 76,598
  • Buuri West 80,762
  • Igembe Central 221,412
  • Igembe North 169,317
  • Igembe South 161,646
  • Imenti North 177,567
  • Imenti South 206,506
  • Meru Central 133,818
  • Tigania Central 104,730
  • Tigania East 72,549
  • Tigania West 139,961
    • Meru National Park 385
    • Mt. Kenya Forest 463

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Ripoti ya makadrio ya mvua kuu ya 2016, Kaunti ya Meru (Kaskazini). Iliwekwa mnamo 2018-04-14.
  2. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
  3. DEVELOPING A SUITABILITY MODEL FOR OPTIMIZED CROPS PRODUCTION. Iliwekwa mnamo 2018-04-14.
  4. TOPO-SEQUENCE ANALYSIS OF CLIMATE VARIABILITY AND LAND USE CHANGES AMONG SMALLHOLDER FARMERS IN MERU COUNTY, KENYA. Jalada kutoka ya awali juu ya 2021-03-08. Iliwekwa mnamo 2018-04-14.
  5. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.