Kaunti ya Meru
Kuhusu makao makuu, tazama Meru
Kaunti ya Meru | |||||
---|---|---|---|---|---|
Kaunti | |||||
Kuro katika Mbuga ya Kitaifa ya Meru | |||||
| |||||
Meru County in Kenya.svg![]() Kaunti ya Meru katika Kenya | |||||
Coordinates: 0°3′N 37°38′E / 0.050°N 37.633°ECoordinates: 0°3′N 37°38′E / 0.050°N 37.633°E | |||||
Nchi | ![]() | ||||
Namba | 12 | ||||
Ilianzishwa | Tarehe 4 Machi, 2013 | ||||
Ilitanguliwa na | Mkoa wa Mashariki | ||||
Makao Makuu | Meru | ||||
Miji mingine | Maua, Nkubu | ||||
Gavana | Kiraitu Murungi, EGH | ||||
Naibu wa Gavana | Titus Ntuchiu Mutea | ||||
Seneta | Mithika Linturi | ||||
Mbunge Mwanamke(Bunge la Taifa) | Kawira Mwangaza | ||||
Bunge la Kaunti | Bunge la Kaunti ya Meru | ||||
Wawakilishi wa Bunge la Kaunti waliochaguliwa | 45 | ||||
Mahakama | Mahakama ya Rufaa, Meru | ||||
Maeneo bunge/Kaunti ndogo | 9 | ||||
Eneo | 6,930.1 km2 (2,675.7 sq mi) | ||||
Idadi ya watu | 1,356,301 | ||||
Kanda muda | Saa za Afrika Mashariki (UTC+3) | ||||
Tovuti | meru.go.ke |
Kaunti ya Meru ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.
Jina lake limetokana na Wameru ambao ndio jamii kubwa zaidi katika kaunti hii.
Sehemu kubwa ya Meru ina ardhi ya rutuba na mvua ya kutosha. Ni kaunti inayojulikana kwa ukuzaji wa miraa, kama zao la biashara. Hata hivyo, ukulima wa ndizi, mahindi, majani ya chai na maharagwe hufanywa[1][2].
Makao makuu yako Meru.
Jiografia[hariri | hariri chanzo]
Kaunti ya Meru inapakana na Kaunti za Nyeri, Laikipia, Tharaka Nithi, Isiolo na Kitui. Iko katika upande wa mashariki mwa Mlima Kenya. Sehemu ya Mbuga ya Kitaifa ya Mlima Kenya iko katika Meru. Mvua yenye kufaa pamoja na udongo wa volkano huwezesha ukulima. Sehemu za Imenti zilizo karibu na Mlima Kenya huwa ni baridi kidogo na zenye vilima. Sehemu za Tigania hazina hali zenye kufaa ukulima isipokuwa karibu na Vilima vya Nyambene, ambapo huwa baridi kidogo. Mbuga ya Kitaifa ya Meru iko katika sehemu za Igembe, kaskazini mashariki mwa kaunti[3].
Mito, k.v. Mto Kathita hutoka Mlima Kenya na Vilima vya Nyambene hutiririsha maji yake ndani ya Mto Tana[4].
Utawala[hariri | hariri chanzo]
Kaunti ya Meru imegawanywa katika maeneo yafuatayo:
Eneo bunge | Wadi |
---|---|
Igembe Kusini | Maua, Kegoi/Antubochiu, Athiru, Gaiti, Akachiu, Kanuni |
Igembe Kati | Akirang’ondu, Athiru, Ruujine, Igembe East Njia, Kangeta |
Igembe Kaskazini | Antuambui, Ntunene, Antubetwe Kiongo, Naathui, Amwathi |
Tigania Magharibi | Athwana, Akithi, Kianjai, Nkomo, Mbeu |
Tigania Mashariki | Thangatha, Mikinduri, Kiguchwa, Mithara, Karama |
Imenti Kaskazini | Municipality, ntima East, Ntima West, Nyaki West, Nyaki East |
Buuri | Timau, Kisima, Kiirua/Naari, Ruiri/Rwarera |
Imenti ya Kati | Mwanganthia, Abothuguchi Central, Abothuguchi West, Kiagu, Kibirichia |
Imenti Kusini | Mitunguu, Igoji East, Igoji West, Abogeta East, Abogeta West, Nkuene |
Meru ni sehemu ya kati ya uliokuwa Mkoa wa Mashariki nchini Kenya upende wa mashariki-kaskazini wa mlima Kenya.
Eneo la Meru lilijumlishwa hadi 1992 katika wilaya ya Meru iliyogawiwa baadaye kuwa wilaya zifuatazo:
- Meru Kati (majimbo ya uchaguzi wa South Imenti, Central Imenti, North Imenti)
- Meru Kaskazini iliyogawiwa tena kuwa wilaya za
- Tigania
- Nyambene (majimbo ya uchaguzi Tigania East, Igembe, Tigania West na Ntonyiri)
- Meru Kusini (jimbo la uchaguzi laitwa Nithi)
- Tharaka
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Kaunti ya Meru: Kilimo cha ndizi kimeizolea sifa - MAKALA - swahilihub.com. Iliwekwa mnamo 2018-04-14.[dead link]
- ↑ Ripoti ya makadrio ya mvua kuu ya 2016, Kaunti ya Meru (Kaskazini). Iliwekwa mnamo 2018-04-14.
- ↑ DEVELOPING A SUITABILITY MODEL FOR OPTIMIZED CROPS PRODUCTION. Iliwekwa mnamo 2018-04-14.
- ↑ TOPO-SEQUENCE ANALYSIS OF CLIMATE VARIABILITY AND LAND USE CHANGES AMONG SMALLHOLDER FARMERS IN MERU COUNTY, KENYA. Iliwekwa mnamo 2018-04-14.
![]() | Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kaunti ya Meru kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |