Kaunti ya Murang'a

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kuhusu mji, soma Murang'a
Kaunti ya Murang'a
Kaunti
Bunge la Kaunti ya Murang'a
Nembo ya Serikali
Murang’a County in Kenya.svg
Kaunti ya Murang'a katika Kenya
Nchi Kenya
Namba21
IlianzishwaTarehe 4 Machi, 2013
Ilitanguliwa naMkoa wa Kati
Makao MakuuMurang'a
Miji mingineMaragua, Kangema
GavanaMwangi wa Iria
Naibu wa GavanaJames Kamau Maina
SenetaIrungu Kang’ata
Mbunge Mwanamke(Bunge la Taifa)Sabina Wanjiru Chege
Bunge la KauntiBunge la Kaunti ya Murang'a
Wawakilishi wa Bunge la Kaunti waliochaguliwa35
Maeneo bunge/Kaunti ndogo7
Eneo2,524.2 km2 (974.6 sq mi)
Idadi ya watu1,056,640
Wiani wa idadi ya watu419
Kanda mudaSaa za Afrika Mashariki (UTC+3)
Tovutimurang'a.go.ke

Kaunti ya Murang'a ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.

Wakati wa sensa ya mwaka 2019 wakazi walikuwa 1,056,640 katika eneo la km2 2,524.2, msongamano ukiwa hivyo wa watu 419 kwa kilometa mraba[1].

Makao makuu yako Murang'a.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Majira ya joto 2022
Reli

Kaunti ya Murang'a imepakana na Nyeri (kaskazini), Embu, Machakos (mashariki), Kiambu (kusini) na Nyandarua (magharibi).

Kaunti hii iko kati ya m 914 na m 3353 juu ya usawa wa bahari wastani. Sehemu za magharibi zimekaribia Milima Aberdare na hivyo kuinuka zaidi. Ina mito kadhaa inayotiririka kutoka vitako vya Milima Aberdare kuelekea magharibi ambapo hutiririsha maji katika Mto Tana.

Murang'a ina vilima na mabonde ambayo huwezesha mito kutiririka. Topografia hii huwa na madhara wakati wa mvua kubwa kwa sababu ya mporomoko wa ardhi.

Udongo wa kaunti hii ni wa volkano ambao una rutuba inayowezesha kilimo. Murang'a huhusika katika kilimo cha kahawa, chai, ng'ombe wa maziwa na miti kama zao la biashara.

Murang'a ina maeneo matatu ya tabianchi:

  • Msitu wa mvua wa tropiki, magharibi karibu na Milima Aberdare
  • Nusutropiki, maeneo ya kati
  • Nusuyabisi, mashariki

Utawala[hariri | hariri chanzo]

Kaunti ya Murang'a imegawiwa katika maeneo bunge yafuatayo:

Eneo bunge/kaunti ndogo Kata
Kangema Kanyenya-Ini, Muguru, Rwathia
Mathioya Gitugi, Kiru, Kamacharia
Kiharu Wangu, Mugoiri, Mbiri, Township, Murarandia, Gaturi
Kigumo Kahumbu, Muthithi, Kigumo, Kangari, Kinyona
Maragua Kimorori/Wempa, Makuyu, Kambiti, Kamahuhu, Ichagaki, Nginda
Kandara Ng'araria, Muruka, Kagundu-Ini, Gaichanjiru, Ithiru, Ruchu
Gatanga Ithanga, Kakuzi/Mitubiri, Mugumo-Ini, Kihumbu-Ini, Gatanga, Kariara

Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [2][hariri | hariri chanzo]

  • Murang'a East 110,311
  • Kangema 80,447
  • Mathioya 92,814
  • Kahuro 88,193
  • Murang'a South 184,824
  • Gatanga 187,989
  • Kigumo 136,921
  • Kandara 175,098
    • Aberdare Forest 43

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
  2. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.