Nenda kwa yaliyomo

Kaunti ya Nyeri

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kaunti ya Nyeri
Kaunti
Kilele cha Lenana katika Mlima Kenya, Kaunti ya Nyeri
Kaulimbiu: ""

Kaunti ya Nyeri katika Kenya
Nchi Kenya
Nambari19
IlianzishwaTarehe 4 Machi, 2013
Ilitanguliwa naMkoa wa Kati
Mji mkuuNyeri
Miji mingineKaratina, Othaya, Kiganjo
Serikali
GavanaEdward Mutahi Kahiga
SenetaEphraim Maina
Mwakilishi wa wanawakeRahab Mukami Wachira
BungeBunge la Kaunti ya Nyeri
Maeneo bunge
Eneo
Jumlakm2 3 325 (sq mi 1 284)
Idadi ya Watu
Jumla759,164
Msongamano228 /km²
Majira ya SaaSaa za Afrika Mashariki (UTC+3)
Tovuti
 nyeri.go.ke

Kaunti ya Nyeri ni mojawapo ya kaunti 47 za Kenya, iliyoko katika eneo la Kati, kwenye miteremko ya magharibi ya Mlima Kenya. Inapakana na Kaunti ya Laikipia kaskazini, Kaunti ya Nyandarua magharibi, Kaunti ya Murang'a kusini, na Kaunti ya Kirinyaga mashariki. Ina idadi ya watu takriban 759,164 kulingana na sensa ya mwaka 2019[1]. Mji wake mkuu na mkubwa ni Nyeri. Nyeri imegawanyika katika maeneo bunge 6: "Tetu, Kieni, Mathira, Othaya, Mukurweini, na Nyeri Mjini". Inajulikana kwa mandhari ya milima, bustani za kahawa na chai, utalii wa asili karibu na Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kenya, pamoja na kuwa eneo la kihistoria la makazi ya Lord Robert Baden-Powell, mwanzilishi wa harakati ya Skauti duniani.

Jiografia

[hariri | hariri chanzo]

Kaunti ya Nyeri imepakana na Laikipia (kaskazini), Kirinyaga (mashariki), Murang'a (kusini) na Nyandarua (magharibi).

Topografia ya kaunti huwa na miinuko mikali na mabonde. Mlima Kenya hupatikana katika mpaka wa Meru na Nyeri. Mto Chania na Mto Sagana ndiyo mito mikubwa ambayo hupitia katika kaunti hii[2].

Kaunti ya Nyeri imegawanyika ifuatavyo[3]:

Eneo bunge/kaunti ndogo Kata
Tetu Dedan Kimathi, Wamagana, Aguthi-Gaaki
Kieni Mweiga, Naromoro, Kiamathaga, Mwiyogo/Endarasha, Mugunda, Gatarakwa, Thegu River, Kabaru, Gakwa
Mathira Ruguru, Magutu, Iriaini, Konyu, Kirimukuyu, Karatina Town
Othaya Mahiga, Iria-ini, Chinga, Karima
Mukurweini Gikondi, Rugi, Mukurwe-ini West, Mukurwe-ini Central
Nyeri Town Kiganjo/Mathari, Rware, Gatitu/Muruguru, Ruring'u, Kamakwa/Mukaro

Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [4]

[hariri | hariri chanzo]
  • Tetu 80,453
  • Kieni East 110,376
  • Kieni West 88,525
  • Mathira East 99,065
  • Mathira West 59,895
  • Nyeri South 91,081
  • Mukurwe-ini 89,137
  • Nyeri Central 140,338
    • Mt. Kenya Forest 188
    • Aberdare Forest 106

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
  2. A REVIEW OF NYERI COUNTY-KENYA STRATEGIC PLAN 2013 – 2017, iliwekwa mnamo 29/04/2018
  3. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-09-04. Iliwekwa mnamo 2021-09-04.
  4. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.