Ruiru
Ruiru | |
Nchi | Kenya |
---|---|
Kaunti | Kiambu |
Idadi ya wakazi | |
- | 238,858 |
Ruiru ni mji wa Kaunti ya Kiambu, ipatikanayo katikati ya Kenya.
Jiografia[hariri | hariri chanzo]
Mji huu uko katika umbali wa takribani kilomita 3 kutoka katika Mpaka wa Nairobi.
Una eneo la km2 292 na umezungukwa na mashamba ya Kahawa. Ruiru ni mmoja kati ya miji inayotambulika zaidi nchini Kenya, ambao unaweza kufikika kwa urahisi kupitia barabara au reli.
Idadi ya Wakazi[hariri | hariri chanzo]
Mji huu umekuwa na ongezeko la idadi ya watu, kutokana na uhaba wa nyumba mjini Nairobi[1].
Mwaka 2009 ulikuwa na wakazi 238,858[2].
Hata hivyo, mji huu umeng'ang'ana kuwatosheleza wakazi wake.
Uchumi[hariri | hariri chanzo]
Wengi wa wakazi wa Ruiru ni wafanyabiashara wenye asili ya Kikuyu.
Mji huu pia una matawi ya benki kadhaa kama vile Benki ya Equity, Benki ya Family, Benki ya Cooperative na Benki ya Barclays.
Pia kuna viwanda mbalimbali katika mji huo.
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- Kituo cha Urekebishaji wa Watoto, Ruiru Archived Machi 12, 2007 at the Wayback Machine.
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ www.earth.columbia.edu
- ↑ Sensa ya Kenya 2009 Archived Januari 9, 2019 at the Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.
Majiranukta kwenye ramani: 1°08′56″S 36°57′25″E / 1.14889°S 36.95694°E
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
![]() | Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Ruiru kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |